Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb) (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma mara baada ya kufanya ziara ofisini hapo tarehe 11 Disemba, 2025. Kulia kwa Waziri Mkuu ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb) na kushoto kwa Waziri Mkuu ni Kamishna wa Maadili Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb) akizungumza na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma (hawapo pichani) katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo jijini Dodoma tarehe 11 Disemba, 2025 mara baada ya kufanya ziara ofisini hapo.
Baadhi ya washiriki wa Mdahalo kuhusu Ukatili wa Watoto wakifutalia kwa makini Mdahalo huo uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Hanang tarehe 5 Disemba, 2025
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya kaskazini Arusha Bw. Gerald Mwaitebele akitoa neno la utangulizi kwa washiriki wa Mdahalo kuhusu Ukatili wa Watoto uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Hanang tarehe 5 Disemba, 2025.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Hanang Bw. Hamad Kaaya akitoa neno kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Hanang katika Mdahalo kuhusu Ukatili wa Watoto uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Hanang tarehe 5 Disemba, 2025.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati- Dodoma Bi. Jasmin Awadhi akitoa mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma katika hafla ya uzinduzi wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa. Halfa hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo tarehe 5 Disemba, 2025.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete(Mb) (katikati) akiambatana na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Regina Qwaray(Mb) (kulia kwa Waziri) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma mara baada ya kufanya ziara ya kikazi ofisi hapo tarehe 26 Novemba, 2025.
Kamishna wa Maadili Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akiwasilisha taarifa ya Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb) (hayupo pichani) katika Ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo jijini Dodoma mara baada ya Waziri huyo kufanya ziara ya kikazi tarehe 26 Novemba,2025.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb) akizungumza na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma (hawapo pichani) katika Ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo jijini Dodoma tarehe 26 Novemba, 2025 mara baada ya kufanya ziara ya kikazi ofisini hapo.
Kamishna wa Maadili, Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua kikao kazi cha kupokea taarifa ya mafunzo ya Maadili kwa viongozi awamu ya kwanza, kikao hicho kimewakutanisha watalamu kutoka Sekretarieti ya Maadili na Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) jijini Arusha katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha IAA tarehe 10 Oktoba, 2025.