Wajumbe wa Menejimenti ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakipewa mafunzo kuhusu e-Mrejesho katika ukumbi wa Ofisi hiyo tarehe 15 Septemba 2023.

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (katikati), Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi, Kamishna wa Maadili (wa kwanza kulia) na viongozi wengine wa kitaifa wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wizara ya Katiba na Sheria na Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu walioteuliwa hivi karibuni baada ya kuapishwa Ikulu, Dar Es Salaam tarehe 14.9.2023

Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi, Kamishna wa Maadili (hayuko pichani) akiongoza kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa Waheshimiwa Majaji wa Rufani na Majaji wa Mahakama Kuu walioteuliwa hivi karibuni katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam tarehe 14.9.2023

Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi, Kamishna wa Maadili (hayuko pichani) akiongoza kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa Katibu Mkuu wa wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Stephene Mbundi, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Balozi Prof. Gatorn Kennedy, Naibu Katibu Mkuu wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Shaib Mussa, Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani na Majaji wa Mahakama Kuu katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam tarehe 14.9.2023.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Lushoto mkoani Tanga Mhe. Mathew Paulo Mbaruku Septemba 6, 2023 akiwa mbele ya Baraza la Maadili jijini Dodoma kujibu tuhuma za ukiukwaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma zinazomkabili.

Wajumbe wa Baraza la Maadili tarehe 6 Septemba, 2023 wakiwa katika kikao cha uchunguzi wa tuhuma za ukiukwaji wa maadili dhidi ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Lushoto mkoani Tanga, Mhe. Mathew Paul Mbaruku (wa kwanza kushoto), katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Dodoma, aliyekaa katikati ni Mwenyekiti wa Baraza Mhe. Jaji (Mst.) Rose Teemba.

Mkuu wa wilaya ya Ulanga Mkoani Morogoro Dkt. Jiulus Kenneth Ningu Septemba 5, 2023 akiwa mbele ya Baraza la Maadili mjini Dodoma kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka.

Mwenyekiti wa Baraza la Maadili Mhe. Jaji (Mst) Rose Teemba (Katikati), Wajumbe wa Baraza, Mawakili wa Serikali na Dkt. Julius Ningu, Mkuu wa wilaya ya Ulanga (wa kwanza kushoto) wakiwa katika kikao cha Baraza la Maadili jijini Dodoma Septemba 5, 2023

Karibu


Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ni Taasisi ya Serikali inayojitegemea chini ya Ofisi ya Rais.Taasisi hii imeanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 132 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya mwaka 1995 iliyotungwa na kuanza kutumika rasmi Julai,1995.

Soma zaidi

  • news title here
    11
    Sep
    2023

    Watumishi wa TRA- Arusha waaswa kuzingatia Ahadi ya Uadilifu

    Watumishi wa TRA- Arusha waaswa kuzingatia Ahadi ya Uadilifu.. Soma zaidi

  • news title here
    05
    Sep
    2023

    DC ULANGA AFIKISHWA MBELE YA BARAZA LA MAADILI KWA TUHUMA ZA MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA

    Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Mkoani Morogoro, Mhe. Dkt. Julius Kenneth Ningu (59) amefikishwa mbele ya Baraza la Maadili kwa tuhuma za ukiukwaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ikiwemo matumizi mabaya ya madaraka na lugha za vitisho dhidi ya watumishi wa umma alipokuwa katika ziara za ukaguzi wa miradi m..... Soma zaidi

  • news title here
    04
    Sep
    2023

    WAHESHIMIWA MAHAKIMU MKOA WA KILIMANJARO WAASWA KUJIEPUSHA NA MGONGANO WA MASLAHI

    Kauli hiyo imetolewa na Katibu Msaidizi kanda ya kaskazini Arusha Bi. Anna Mbasha alipokuwa akitoa mafunzo kwa mahakimu wa ngazi mbalimbali wa mkoa wa Kilimanjaro kuhusu maadili hivi karibuni... Soma zaidi

Habari Zaidi
    • 27
      Jul
      2017

      Sekretarieti ya Maadili yaadhimisha Siku ya Maadili.

      Mahali: At Mnazi Mmoja Stadium

      Soma zaidi
    • 29
      Jul
      2017

      maadili siku ya michezo

      Mahali: Gymkhana Ground

      Soma zaidi
    • 25
      Jul
      2017

      Warsha ya Wahariri wa Vyombo vya Habari

      Mahali: Serena Hotel

      Soma zaidi
    • 25
      Jul
      2017

      Baraza la Maadili

      Mahali: Karimjee Hall

      Soma zaidi
    Matukio Zaidi