Walimu Wakuu wa shule za msingi Wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma wakifatilia mada kuhusu umuhimu wa klabu za maadili mashuleni kutoka kwa Afisa Maadili Bw. Joshua Mwambande (hayupo pichani) katika ukumbi wa shule ya sekondari Mpwapwa tarehe 25 Aprili, 2025.
Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati-Dodoma Bi. Philipina Kobelo akitoa elimu ya maadili kwa wanafunzi wa shule ya msingi Nana iliyopo wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma wakati wa uzinduzi wa klabu mpya ya maadili shuleni hapo tarehe 24 Aprili, 2025.
Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kan-da ya Kati Bi. Judith Danford akitoa elimu ya Maadili kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Solya iliyopo wilayani Manyoni mkoani Singida katika zoezi la uzinduzi wa klabu ya Maadili shuleni hapo tarehe 24 Aprili, 2025. Kanda ya Kati inaendelea na zoezi la kuhuisha na kufungua klabu mpya za Shule ya Msingi na Sekondari.
Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Chuo cha Uhasibu Arusha wakisikiliza mada kuhusu Maadili ya Viongozi wa Umma iliyotolewa na Katibu Msaidizi Kanda ya Kaskazini Bw. Gerald Mwaitebele (hayupo pichani) kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika tarehe 23 Aprili, 2025 katika ukumbi wa Chuo hicho.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Bi. Mwanahamisi Ally akizungumza na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati-Dodoma (hawapo pichani). Maafisa hao wamefika ofisini hapo tarehe 23 Aprili, 2025 kwa ajili ya kupata idhini ya kutembelea baadhi ya klabu za maadili zilizopo wilayani humo.
Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kanda ya Kati Bw. Christian Kapere akitoa elimu ya maadili kwa wanachama wa klabu ya Maadili ambao ni wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mwasi iliyopo wilayani Manyoni mkoani Singida, Kanda ya Kati inaendelea na zoezi la kuhuisha na kufungua klabu mpya za Shule ya Msingi na Sekondari, zoezi hilo lilifanyika tarehe 23 Aprili, 2025.
Mhe. Mussa Bohero Jangwa Diwani wa Kata ya Mayomboni mkoani Tanga akiwa mbele ya Baraza la Maadili tarehe 27 Machi, 2025 kwa tuhuma za kushindwa kuwasilisha Tamko la Raslimali na Madeni kwa Kamishna wa Maadili kwa mujibu wa sheria ya Maadili. Tuhuma ambazo Mhe Mussa amekiri hivyo Baraza limemkuta na hatia
Mhe. Cleophas John Mziray Hakimu Mahakama ya Mwanzo Puge mkoani Tabora akiwa mbele ya Baraza la Maadili tarehe 27 Machi, 2025 kwa tuhuma za kushindwa kuwasilisha Tamko la Raslimali na Madeni kwa Kamishna wa Maadili kwa mujibu wa sheria ya Maadili. Tuhuma ambazo Mhe. Cleophas amekiri hivyo Baraza limemkuta na hatia.
Mhe. Mwandei Machumwa Mohamed Diwani wa Kata ya Mkinga mkoani Tanga akiwa mbele ya Baraza la Maadili tarehe 27 Machi, 2025 kwa tuhuma za kushindwa kuwasilisha Tamko la Raslimali na Madeni kwa Kamishna wa Maadili kwa mujibu wa sheria ya Maadili. Tuhuma ambazo Mhe Mwandei amekiri hivyo Baraza limemkuta na hatia.
Mhe. Mwandei Machumwa Mohamed, Diwani wa Kata ya Mkinga mkoani Tanga akiwa mbele ya Baraza la Maadili tarehe 27 Machi, 2025 kwa tuhuma za kushindwa kuwasilisha Tamko la Raslimali na Madeni kwa Kamishna wa Maadili kwa mujibu wa sheria ya Maadili. Tuhuma ambazo Mhe Mwandei amekiri hivyo Baraza limemkuta na hatia