Wadau wa masuala ya maadili wakiwa katika mdahalo kuhusu changamoto za kimaadili kwa Wanafunzi katika shule za msingi na sekondari. Mdahalo huo umefanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru mkoani Arusha tarehe 26 Agosti, 2025.
Bw. Gerald Mwaitebele Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini-Arusha akifungua Mdahalo kuhusu changamoto za kimaaadili kwa Wanafunzi na ufumbuzi wake. Mdahalo huo umefanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru mkoani Arusha tarehe 26 Agosti,2025 kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali.
Mwenyekiti na Wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (Tan Trade) wakila Kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwenye uzinduzi wa Bodi hiyo katika ukumbi wa Kilimanjaro uliopo uwanja wa Mwl. J.K Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 22 Agosti, 2025.
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Tumbaku Tanzania (TTB) Bw. Stanley Mnozya akifungua mafunzo kuhusu Sheria ya Maadili kwa Watumishi wa Bodi hiyo (hawapo pichani) katika ukumbi wa mikutano wa Nyerere uliopo hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza tarehe 14 Agost, 2025.
Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Fabian Pokela akitoa mada kuhusu Sheria ya Maadili kwa Watumishi wa Bodi ya Tumbaku Tanzania (hawapo pichani) katika mafunzo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Nyerere uliopo hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza tarehe 14 Agosti, 2025
Makamu Mwanyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) Mhe. Mohamed Khamis Hamad akipata maelezo kutoka kwa Katibu Msaidizi Idara ya Ukuzaji Maadili Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Salvatory Kilasara, alipotembelea banda la ofisi hiyo kwenye Maonesho ya Nanenane viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma tarehe 7 Agosti, 2025.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jabiri Bakari akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Banda la Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi ya Umma katika Maonesho ya Sikukuu ya wakulima Nanenane tarehe 5 Agosti, 2025 yanayofanyika kitaifa jijini Dodoma.
Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Dkt. Vicent Mashinji akipata maelezo kutoka kwa Katibu Msaidizi Idara ya Ukuzaji Maadili Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Salvatory Kilasara alipotembelea banda la ofisi hiyo kwenye Maonesho ya Nananane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni tarehe 4 Agosti, 2025.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati Dodoma Bi. Jasmin Awadhi akitoa elimu ya Maadili kwa Wananchi waliotembelea banda la ofisi hiyo katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma tarehe 3 Agosti, 2025.
Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Christian Kapere akielezea majukumu ya ofisi hiyo kwa wananchi waliotembelea banda la ofisi hiyo katika maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma tarehe 02 Agosti, 2025.