Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi (hayupo pichani) akiongoza kiapo cha ahadi ya uadilifu kwa viongozi mbalimbali walioteuliwa hivi karibuni. Kutoka Kulia ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Bw. Emmanuel Tutuba akifuatiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Natu El-Maamry pamoja na Katibu wa Tume ya Kurekebisha sheria Bw. Griffin Mwakapeje. Tukio hilo lilifanyika Ikulu Chamwino-Dodoma tarehe 09 Januari,2023.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama (Mb) akitoa maelekezo mara baada ya kutembelea ujenzi wa jengo la Ofisi la Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Dodoma hivi karibuni. Kushoto kwa Mhe Waziri ni Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi.Wengine katika picha ni watendaji kutoka Wakala wa Majengo Tanzania.
Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akitoa hotuba yake katika maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu iliyofanyika katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma tarehe 10 Desemba,2022.
Waziri wa Nchi, Ofis ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama (Mb) akitoa neno la ukaribisho kwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yaliyofanyika tarehe 10 Desemba,2022 katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi akitoa maelezo mafupi katika maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu iliyofanyika katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma tarehe 10 Desemba,2022.
Kaimu Katibu Msaidizi Kanda ya Magharibi -Tabora Bw. Patrick Shayo (wa tatu kutoka kushoto) pamoja na Naibu Kamanda wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa Mkoa wa Tabora Bw. Daudi Ndyamukama (wa nne kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na wanachama wa klabu za maadili na klabu za wapinga rushwa kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma-Tabora, Chuo chja Ardhi-Tabora na Chuo cha Ufugaji Nyuki mara baada ya kuhitimisha kongamano la kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tabora tarehe 10 Desemba 2022.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akitoa hotuba ya ufunguzi wa siku ya Maadili na Haki za Binadamu nchini. Uzinduzi huo ulifanyika katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma tarehe 06 Desemba,2022.
Kulia kwa Mhe. Waziri ni Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi na kushoto kwa Mhe. Waziri ni Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bi. Neema Mwakalyelye.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akipata melekezo kutoka kwa Maafisa wa Sekretarieti ya Maadili ya viongozi wa Umma alipotembelea banda la Ofisi hiyo katika ufunguzi wa maadhimisho ya siku ya maadili na haki za binadamu nchini iliyofanyika katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma tarehe 06 Desemba 2022
Karibu
Sekretarieti ya Maadili ni Idara ya huru ya Serikali chini ya Ofisi ya Rais iliyoanzishwa chini ya Ibara ya 132 ya Katiba ya 1977 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kazi yake kuu ni kutekeleza Sheria ya Maadili ya Uongozi wa Umma, Na. 13 ya 1995 (Sura ya 398), hasa kufuatilia tabia na maadili ya Viongozi wa Umma. Tovuti hii ni njia ya habari muhimu juu ya kukuza na kutekeleza kanuni na maadili ya kimaadili ambayo ni lazima ya kuzingatiwa na Viongozi wote wa Umm...
Soma zaidi
-
12
Dec
2022
Viongozi wa Umma watakiwa kutimiza Ahadi ya Uadilifu
Viongozi wa Umma watakiwa kutimiza Ahadi ya Uadilifu..
Soma zaidi
-
06
Dec
2022
Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu nchini yazinduliwa rasmi
Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu nchini yazinduliwa rasmi..
Soma zaidi
-
08
Nov
2022
Rasimu ya mkataba wa huduma kwa mteja kujadiliwa.
Rasimu ya mkataba wa huduma kwa mteja kujadiliwa...
Soma zaidi
Habari Zaidi
-
27
Jul
2017
Sekretarieti ya Maadili yaadhimisha Siku ya Maadili.
Mahali: At Mnazi Mmoja Stadium
Soma zaidi
-
29
Jul
2017
maadili siku ya michezo
Mahali: Gymkhana Ground
Soma zaidi
-
25
Jul
2017
Warsha ya Wahariri wa Vyombo vya Habari
Mahali: Serena Hotel
Soma zaidi
-
25
Jul
2017
Baraza la Maadili
Mahali: Karimjee Hall
Soma zaidi
Matukio Zaidi