Afisa TEHAMA, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Francis Toke akitoa Mada kuhusu Ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (0nline Declaration System-ODS) katika mafunzo ya Viongozi wa Umma yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara tarehe 17 Desemba 2024.
Baadhi ya Viongozi wa mkoa wa Mara walioshiriki katika mafunzo kuhusu Maadili ya Viongozi wa umma wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi (hayupo pichani) ktika mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara tarehe 17 Desemba 2024.
Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi akifungua mafunzo ya Maadili ya viongozi wa Umma mkoani humo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa tarehe 17 Desemba 2024.
Katibu Msaidizi Idara ya Ukuzaji wa Maadili, Bw. Salvatory Kilasara akitoa elimu ya uzingatiaji wa Maadili pamoja na ya ujazaji wa Tamko la Raslimali na Madeni kwa njia ya Mtandao (ODS) kwa viongozi wa Umma wa mkoani Ruvuma wakati wa kikao kazi kilichofanyika ukumbi wa Bomba mbili tarehe 17 Desemba, 2024 mjini Songea. Viongozi walioshiriki ni Kamati ya Usalama ya Mkoa na Wilaya, wakuu wa Taasisi zilizopo Ruvuma, Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri za Mkoa wa Ruvuma.
Mhe. Halima Dedendego, Mkuu wa Mkoa wa Singida akiongea na baadhi ya watumishi wa mkoa wa Singida katika Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu lililofanyika tarehe 10.12.2024 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati- Dodoma Bi. Jasmin Awadhi akitoa neno la utangulizi katika kongamano la siku ya Maadili na Haki za Binadamu. Kongamano hilo lilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Singida Disemba 10,2024.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mhe. Jaji (Stahiki) Mathew Mwaimu akifungua kongamano la siku ya Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa ambalo limefanyika ukumbi wa PSSSF jijini Dodoma tarehe 10 Disemba, 2024. Mhe. Mathew ni mgeni rasmi wa kongamano hilo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (Mb) akiongea na waandishi wa Habari wakati akizindua Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu Kitaifa mwaka 2024. Hafla ya uzinduzi huo ulifanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi tarehe 5 Disemba, 2024. Kulia kwa Mhe. Waziri ni Bw. Mululi Mahendeka, Katibu Mkuu Ikulu na kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mhe. Jaji (Stahiki) Mathew Mwaimu.
Ndugu Kiongozi, Sekretarieti ya Maadili inapokea Tamko la Raslimali, Maslahi na Madeni kwa njia ya mtandao (Online Declaration System-ODS.) kuanzia tarehe 1 Oktoba hadi 31 Disemba, 2024.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Mst) Sivangilwa Mwangesi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya awali kwa watumishi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Ofisi hiyo Jijini Dodoma tarehe 11 Novemba,2024. Kulia kwa Kamishna ni Katibu Idara ya Ukuzaji Maadili Bw. Waziri Kipacha na kushoto kwa Kamishna ni Katibu Idara ya Uzingatiaji Maadili Bw. Kassim Mkwawa.