Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi akifuatilia maelezo yanayotolewa na Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya kati Bi. Jasmin Awadhi kuhusu Maadili kwa viongozi wa umma. Tukio hilo lilitokea tarehe 26 Juni, 2025 wakati Waziri Lukuvi akizindua Bodi ya wadhamini ya mfuko wa udhamini wa kudhibiti UKIMWI ofisini kwake jijini Dodoma.
Wajumbe wa Bodi ya wadhamini ya mfuko wa udhamini wa kudhibiti UKIMWI wakitoa Ahadi ya Uadilifu mbele ya Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya kati Bi. Jasmin Awadhi (Hayupo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo iliyofanyika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) tarehe 26 Juni, 2025.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Clement Sangu (Mb) aliyesimama mbele akipata maelezo kwa namna Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inavyotekeleza majukumu yake, kutoka kwa Afisa wa ofisi hiyo Bi. Desderia Haule (aliyeshika kipaza sauti), alipotembelea banda la ofisi hiyo katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma tarehe 20 Juni, 2025.
Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Kihenzile (Mb) aliyesimama kulia akipata maelezo kuhusu majukumu ya Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka kwa Afisa wa ofisi hiyo Bi. Desderia Haule (wa kwanza kushoto), alipotembelea banda la ofisi hiyo katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma tarehe 19 Juni, 2025.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi akisaini kitabu cha wageni katika banda la Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma tarehe 18 Juni, 2025.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bi. Desderia Haule akielezea majukumu ya ofisi hiyo kwa Dkt. Adolar Duwe ambaye ni Meneja wa Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Utawala kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) alipotembelea banda la ofisi hiyo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma tarehe 16 Juni, 2025.
Mwenyekiti wa Baraza la Maadili, Mhe. Jaji (Mst.) Rose Teemba akimkabidhi Tuzo Bw. Peter Ilomo mjumbe wa Baraza la Maadili aliyemaliza muda wake wa kulitumikia Baraza. Tukio hilo limefanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma tarehe 16 Juni, 2025 jijini Dodoma.