Katibu Idara ya Ukuzaji Maadili, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Waziri Kipacha akitoa neno la ufunguzi wa kikao kazi cha kuhuisha makosa ya ukiukwaji wa Maadili kwa Viongozi wa Umma. Kikao kazi hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Sekretarieti ya Maadili mkoani Morogoro tarehe 28 Novemba, 2023.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Skretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bi. Emma Gelani akitoa neno la utangulizi katika ufunguzi wa kikao kazi cha kuhuisha makosa ya ukiukwaji wa maadili kwa Viongozi wa Umma. Kikao kazi hicho kilifanyika katika ukumbi wa Ofisi za Sekretarieti ya Maadiili Mkoani Morogoro tarehe 28 Novemba,2023.
Afisa Maadili kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bi. Modesta Mtui akiongoza kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi mbalimbali kutoka Benki kuu ya Tanzania (BOT). Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Ofisi za Benki kuu ya Tanzania Dodoma tarehe 24 Novemba,2023
Bw. Waziri Kipacha, Katibu Ukuzaji Maadili Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma akifungua mafunzo kwa wajumbe wa Baraza la Maadili (hawako pichani) tarehe 6 Novemba, 2023 katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Point Zone Resort jijini Arusha.
Katibu Msaidizi Kanda ya Magharibi Tabora Bw Gerald Mwaitebele akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Klabu ya Maadili na wanachama wa Klabu hiyo katka shule ya Sekondari yay a Kanyenye iliyoko Mkoani Tabora tarehe 2 Novemba 2023.
Mkuu wa Wilaya ya Ngara Kanali Mathias Kahabi akifungua mafunzo ya Maadili kwa Viongozi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara . Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoliki Rulenge Wilayani Ngara Mkoani Kagera tarehe 02 Novemba,2023
Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Ziwa - Mwanza Bw. Godson Kweka akitoa neno la utangulizi katika mafunzo ya Maadili kwa Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara . Mafunzo hayo yalifanyika katika Ukumbi wa Kanisa Katoliki Rulenge Wilayani Ngara Mkoani Kagera tarehe 02 Novemba, 2023
Afisa Maadili Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kanda ya Ziwa Bw. Shaban Shirima akitoa mada ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoliki Ruleje Wilayani Ngara tarehe 02 Novemba,2023
Washiriki wa mafunzo ya Maadili ambao ni viongozi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Ngara wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo Mafunzo hayo yalifanyika katika Ukumbi wa Kanisa Katoliki Rulenge Wilayani Ngara Mkoani Kagera tarehe 02 Novemba, 2023
Mkurugenzi wa Utawala na Raslimaliwatu Bi Teddy Njau akitoa Neno la Ufunguzi katika kikao cha kuandaa Mtaala wa Mafunzo kwa Wachunguzi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, tarehe 1 Novemba 2023.