JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Historia

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ni Idara ya Serikali inayojitegemea chini ya Ofisi ya Rais iliyopewa mamlaka ya kuchunguza tabia na mwenendo wa kiongozi wa umma yeyote kwa madhumuni ya kuhakikisha kuwa masharti ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma yanazingatiwa ipasavyo. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ilianzishwa chini ya Ibara ya 132 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

Sekretarieti ya Maadili imepewa mamlaka ya kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya 1995 sura 398. Sheria hii ilianza kutumika tarehe 01 Julai 1995 na inatumika Tanzania Bara pamoja na Zanzibar kwa viongozi wenye madaraka katika Serikali ya Muungano.

Sekretarieti ya Maadili inaongozwa na Kamishna wa Maadili ambaye huteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, Rais huwezesha kupatikana kwa watumishi wengine wa Sekretarieti ya Maadili ambao huwajibika kula kiapo cha kutunza siri zinazohusiana na majukumu ya taasisi.

Taasisi ina ofisi ya Makao Makuu iliyopo Dodoma pamoja na ofisi nane za Kanda kama ifuatavyo;

  • Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yenye mikoa ya Mbeya, Iringa, Katavi, Songwe, Njombe na Rukwa.
  • Kanda ya Kusini yenye mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma.
  • Kanda ya Kati yenye mikoa ya Dodoma na Singida.
  • Kanda ya Kaskazini yenye mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara.
  • Kanda ya Magharibi yenye mikoa ya Tabora, Kigoma, Simiyu na Shinyanga.
  • Kanda ya Ziwa yenye mikoa ya Mwanza, Mara, Geita na Kagera.
  • Kanda ya Mashariki yenye mikoa ya Tanga na Morogoro.
  • Kanda Maalum yenye mikoa ya Dar Es Salaam na Pwani pamoja na Unguja na Pemba.

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >