Baadhi ya Makatibu na Manaibu Makatibu wakuu wa wizara wakifuatilia kwa makini mafunzo ya maadili kwa makatibu na manaibu makatibu wakuu wa Wizara. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Sanaan jijini Dodoma tarehe 20 Februari, 2026.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akitoa neno la utambulisho katika mafunzo ya maadili kwa makatibu na manaibu makatibu wakuu wa Wizara. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Sanaan jijini Dodoma tarehe 20 Februari, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Ikulu (Kazi Maalum) Mhe. Palamagamba Kabudi (Mb) akifungua mafunzo ya maadili kwa makatibu na manaibu makatibu wakuu wa Wizara. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Sanaan jijini Dodoma tarehe 20 Februari, 2026.
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Geita walioshiriki mafunzo ya maadili wakifuatilia mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo yalifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita tarehe 20 Februari, 2026.
Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais, Sekretaieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Kanda ya Ziwa Bw. Godson Kweka akitoa mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa Viongozi wa Mkoa wa Geita (hawapo pichani) katika mafunzo ya maadili yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita tarehe 20 Februari, 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela akitoa neno la utangulizi katika mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Mkoa huo (hawapo pichani). Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita tarehe 20 Februari, 2026.
Baadhi ya Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba walioshiriki mafunzo ya maadili wakifuatilia mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo iliyopo mkoani Dodoma tarehe 14 Februari, 2026.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Bw. Raphael Lebba akitoa neno la utangulizi katika mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Halmashauri hiyo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo iliyopo mkoani Dodoma tarehe 14 Februari, 2026.
Katibu Msaidizi, Sekretaieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Kanda ya Kati-Dodoma Bi. Jasmin Awadhi akitoa mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba (hawapo pichani) katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kimaadili Viongozi hao yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo iliyopo mkoani Dodoma tarehe 14 Februari, 2026.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray (Mb) akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria (hawapo pichani), wakati wa kikao na kamati hiyo kilichofanyika katika ofisi za Bunge jijini Dodoma tarehe 12 Februari, 2026.