Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati. Bi. Jasmin Awadh akitoa mada kuhusu Sheria ya maadili kwa Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma katika mafunzo ya maadili yaliyofanyika ukumbi wa Zabibu Hotel mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma wakifuatilia mada mbalimbali za maadili wakati wa mafunzo ya maadili yaliyofanyika katika ukumbi wa Zabibu Hotel Mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya sheria ya Maadili wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Zabibu Hotel Mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Maafisa Ununuzi na Ugavi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma walifatilia hotuba ya mgeni rasmi katika kikao hicho kilichofanyika tarehe 27 Aprili, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi mkoani Singida.
Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi na Manunuzi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Kenedy Mwakalindile akitoa neno la utangulizi katika kikao kazi cha Maafisa Ununuzi na Ugavi wa ofisi hiyo kilichofanyika tarehe 27 Aprili, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) mkoani Singida
Kamishna wa Maadili Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua kikao kazi cha Maafisa Ununuzi na Ugavi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika tarehe 27 Aprili, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) mkoani Singida.
Mratibu wa mafunzo ya Maadili na Uadilifu kwa Viongozi wa Umma kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Dkt. Birigitha Ngwano John akitoa neno la ufunguzi katika mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya MORENA mkoani Morogoro tarehe 22 April, 2026.
Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa shule za msingi na sekondari wa Mkoa wa Manyara ambao ni walezi wa klabu za maadili mara baada ya mafunzo ya maadili kwa walimu hao yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.
Baadhi ya walimu kutoka shule za msingi na sekondari mkoani Manyara wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya maadili kwa walimu walezi wa klabu za maadili kutoka shule za Mkoa wa Manyara yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.
Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji akifungua mafunzo ya maadili kwa walimu walezi wa klabu za maadili kutoka shule za mkoani Manyara yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.