Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kusini Bw. Philoteus Manula akifungua kikao kazi kwa wawakilishi wa vyombo vya habari kutoka Kanda ya Kusini kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kanda hiyo tarehe 10 Aprili, 2026.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi ambao ni wamiliki, wahariri na waandishi mbalimbali wa habari kutoka mkoani Tanga wakifuatilia mijadala mbalimbali. Kikao kazi hicho kilifanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Bandari mkoani Tanga tarehe 10 Aprili,2026.
Baadhi ya wadau wa habari kutoka mikoa ya Pwani na DaresSalaam walioshiriki Kikao kazi kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika kukuza maadili nchini wakifatilia mada mbali mbali katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Shule ya Uongozi Mwalimu Nyerere mjini Kibaha mkoani Pwani tarehe 09 Aprili, 2026.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda Maalum Bi. Elizabeth Komba akifungua Kikao Kazi cha wamiliki, wahariri na waandishi wa habari wa Kanda hiyo. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Shule ya Uongozi Mwalimu Nyerere mjini Kibaha mkoani Pwani tarehe 09 Aprili, 2026.
Afisa Maadili kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kanda ya Mashariki Bw. Seleman Seleman akiwasilisha mada kuhusu majukumu ya Taasisi katika kikao kazi na wahariri pamoja na waandishi mbalimbali wa vyombo vya habari kutoka mkoani Morogoro. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Hazina Ndogo mkoani Morogoro tarehe 8 Aprili, 2026.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha ambao ni wahariri na waandishi mbalimbali wa habari kutoka mkoani morogoro wakifuatilia mijadala mbalimbali. Kikao kazi hicho kilifanyika katika ukumbi wa hazina ndogo mkoani Morogoro tarehe 8 Aprili, 2026.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Ziwa Bw. Godson Kweka akieleza majukumu ya Sekretarieti ya Maadili kwa wadau wa habari kutoka mikoa ya Kanda hiyo. Kikao kazi hicho kilifanyika mkoani Geita tarehe 31 Machi, 2026.
Baadhi ya wadau wa habari wa mikoa ya Kanda ya Kati walioshiriki kikao kazi kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika kukuza maadili nchini wakisikiliza kwa makini hotuba ya ufunguzi katika kikao kazi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Zabibu Hoteli iliyopo jijini Dodoma tarehe 01 April, 2026.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati Bi. Jasmin Awadh akifungua kikao kazi na wadau wa habari wa mikoa ya Kanda hiyo. Kikao kazi hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Zabibu Hotel iliyopo mkoani Dodoma tarehe 01 Aprili, 2026.
Baadhi ya wadau wa habari walioshiriki Kikao kazi kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika kukuza maadili nchini wakifatilia mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Midland iliyopo Makambako mkoani Njombe tarehe 30 Machi, 2026.