Wanafunzi wa Shule ya msingi Blessed Mabuba ya jijini Dodoma wakipata elimu ya maadili, kutoka kwa Afisa Maadili wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bw. Anno Mgani, walipotembelea banda la Ofisi hiyo katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma, tarehe 6 Agosti, 2026.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bw. Anno Mgani akitoa elimu ya maadili kwa wadau waliotembelea banda la ofisi hiyo katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma tarehe 5 Agosti, 2026.
Wadau wakipata elimu ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka kwa Maafisa wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, walipotembelea banda la ofisi hiyo katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma tarehe 4 Agosti, 2026.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Zuzu ya jijini Dodoma wakipata elimu ya maadili, kutoka kwa Afisa Maadili wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bw. Marcus Mawanga, walipotembelea banda la Ofisi hiyo katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma, tarehe 3 Agosti, 2026.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bw. Patience Ntwina akipata maelezo jinsi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inavyofanya kazi kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bw. Honoratus Ishengoma alipotembelea Banda la Maadili tarehe 10 Julai, 2026 wakati wa Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar-es-Salaam.
Wanafunzi wa sekondari ya Wasichana Nangwa iliyopo wilayani Hanang mkoani Manyara wakifatilia kwa makini mada ya misingi ya maadili kutoka kwa Afisa wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini Bw. Musiba Magoma (hayupo pichani) wakati wa zoezi la kutembelea Klabu za Maadili wilayani humo lililofanyika tarehe 19 Mei, 2026.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya sheria ya Maadili wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Zabibu Hotel Mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.
Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa shule za msingi na sekondari wa Mkoa wa Manyara ambao ni walezi wa klabu za maadili mara baada ya mafunzo ya maadili kwa walimu hao yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.
Baadhi ya walimu kutoka shule za msingi na sekondari mkoani Manyara wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya maadili kwa walimu walezi wa klabu za maadili kutoka shule za Mkoa wa Manyara yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.
Baadhi ya wadau wa habari kutoka mikoa ya Pwani na DaresSalaam walioshiriki Kikao kazi kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika kukuza maadili nchini wakifatilia mada mbali mbali katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Shule ya Uongozi Mwalimu Nyerere mjini Kibaha mkoani Pwani tarehe 09 Aprili, 2026.