Dkt. Dotto Bulendu kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine-Mwanza akitoa mada ya utoaji elimu kwa umma kupitia Redio kwa maafisa wa Sekretarieti ya Maadili ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka makao makuu na Kanda wakati wa mafunzo ya kukuza maadili kupitia vyombo vya habari yaliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Flomi mjini Morogoro tarehe 4 Mei, 2026.
Dkt. Elbert Mkoko kutoka Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam akitoa mada ya namna ya uwasilishaji mada katika hadhira mbalimbali kwa maafisa wa Sekretarieti ya Maadili ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka makao makuu na Kanda wakati wa mafunzo ya kukuza maadili kupitia vyombo vya habari yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Flomi mjini Morogoro tarehe 4 Mei, 2026.
Kamishna wa Maadili, Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya kukuza maadili kupitia vyombo vya habari kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma makao makuu na Kanda yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Flomi mjini Morogoro tarehe 4 Mei, 2026.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati. Bi. Jasmin Awadh akitoa mada kuhusu Sheria ya maadili kwa Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma katika mafunzo ya maadili yaliyofanyika ukumbi wa Zabibu Hotel mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma wakifuatilia mada mbalimbali za maadili wakati wa mafunzo ya maadili yaliyofanyika katika ukumbi wa Zabibu Hotel Mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya sheria ya Maadili wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Zabibu Hotel Mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Maafisa Ununuzi na Ugavi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma walifatilia hotuba ya mgeni rasmi katika kikao hicho kilichofanyika tarehe 27 Aprili, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi mkoani Singida.
Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi na Manunuzi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Kenedy Mwakalindile akitoa neno la utangulizi katika kikao kazi cha Maafisa Ununuzi na Ugavi wa ofisi hiyo kilichofanyika tarehe 27 Aprili, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) mkoani Singida
Kamishna wa Maadili Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua kikao kazi cha Maafisa Ununuzi na Ugavi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika tarehe 27 Aprili, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) mkoani Singida.
Mratibu wa mafunzo ya Maadili na Uadilifu kwa Viongozi wa Umma kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Dkt. Birigitha Ngwano John akitoa neno la ufunguzi katika mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya MORENA mkoani Morogoro tarehe 22 April, 2026.