Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wapya wa Ofisi ya Rasi, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma baada ya ufunguzi wa mafunzo elekezi kwa watumishi hao yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2026.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bi. Teddy Njau, akitoa neno la utangulizi kwa washiriki wa mafunzo elekezi kwa watumishi wapya (hawapo pichani). Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2025.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi, akifungua mafunzo elekezi kwa watumishi wapya (hawapo pichani) wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2026.
Wanafunzi wa Shule ya msingi Blessed Mabuba ya jijini Dodoma wakipata elimu ya maadili, kutoka kwa Afisa Maadili wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bw. Anno Mgani, walipotembelea banda la Ofisi hiyo katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma, tarehe 6 Agosti, 2026.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bw. Anno Mgani akitoa elimu ya maadili kwa wadau waliotembelea banda la ofisi hiyo katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma tarehe 5 Agosti, 2026.
Wadau wakipata elimu ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka kwa Maafisa wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, walipotembelea banda la ofisi hiyo katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma tarehe 4 Agosti, 2026.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Zuzu ya jijini Dodoma wakipata elimu ya maadili, kutoka kwa Afisa Maadili wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bw. Marcus Mawanga, walipotembelea banda la Ofisi hiyo katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nanenane) yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma, tarehe 3 Agosti, 2026.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bw. Patience Ntwina akipata maelezo jinsi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inavyofanya kazi kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bw. Honoratus Ishengoma alipotembelea Banda la Maadili tarehe 10 Julai, 2026 wakati wa Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar-es-Salaam.
Wanafunzi wa sekondari ya Wasichana Nangwa iliyopo wilayani Hanang mkoani Manyara wakifatilia kwa makini mada ya misingi ya maadili kutoka kwa Afisa wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini Bw. Musiba Magoma (hayupo pichani) wakati wa zoezi la kutembelea Klabu za Maadili wilayani humo lililofanyika tarehe 19 Mei, 2026.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya sheria ya Maadili wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Zabibu Hotel Mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.