Msuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi, Bw. Erastus Mtui ametoa wito kwa watumishi waliopo kwenye Taasisi anayongoza kuzingatia Maadili na kujiepusha na Mgongano wa Maslahi wanapotekeleza majukumu yao, Bw. Mtui ametoa wito huo wakati akifunga mafunzo ya Maadili yaliyotolewa na Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili Viongozi wa Umma katika ofisi za Taasisi hiyo zilizopo mji wa Serikali mkoani Dodoma tarehe 16 Mei, 2025.
Viongozi na watumishi kutoka Taasisi ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi wakiongozwa na Msuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi, Bw. Erastus Mtui (aliyekaa kiti cha mbele) wakifuatilia mada ya mgongano wa Maslahi inayotolewa na Afisa kutoka Sekretarieti ya Maadili, Bw. Christian Kapere. Elimu hiyo imetolewa na katika ofisi za Taasisi hiyo zilizopo mji wa Serikali mkoani Dodoma tarehe 16 Mei, 2025.
Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Fabian Pokela hayupo pichani, akiongoza kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa baadhi ya Viongozi kutoka katika Taasisi mbali mbali nchini mara baada ya mafunzo ya Maadili yaliyofanyika katika ukumbi wa Golden Crest Hotel iliyopo Jijini Arusha tarehe 14 Mei,2025.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati-Dodoma Bw. Alfred Mboya akitoa elimu ya maadili kwa Wanafunzi wa shule ya msingi Mautya iliyopo wilayani Kongwa mkoani Dodoma wakati wa uzinduzi wa klabu mpya ya maadili shuleni hapo tarehe 14 Mei, 2025.
Afsa Maadili Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Ziwa-Mwanza Bw. Innocent Shetui akitoa mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa Viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo tarehe 8 Mei, 2025.
Baadhi ya Viongozi walioshiriki katika mafunzo kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakimsikiliza mtoa mada Bw. Innocent Shetui (hayupo pichani). Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba tarehe 8 Mei, 2025.
Walimu Wakuu wa shule za msingi Wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma wakifatilia mada kuhusu umuhimu wa klabu za maadili mashuleni kutoka kwa Afisa Maadili Bw. Joshua Mwambande (hayupo pichani) katika ukumbi wa shule ya sekondari Mpwapwa tarehe 25 Aprili, 2025.
Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati-Dodoma Bi. Philipina Kobelo akitoa elimu ya maadili kwa wanafunzi wa shule ya msingi Nana iliyopo wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma wakati wa uzinduzi wa klabu mpya ya maadili shuleni hapo tarehe 24 Aprili, 2025.
Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kan-da ya Kati Bi. Judith Danford akitoa elimu ya Maadili kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Solya iliyopo wilayani Manyoni mkoani Singida katika zoezi la uzinduzi wa klabu ya Maadili shuleni hapo tarehe 24 Aprili, 2025. Kanda ya Kati inaendelea na zoezi la kuhuisha na kufungua klabu mpya za Shule ya Msingi na Sekondari.
Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Chuo cha Uhasibu Arusha wakisikiliza mada kuhusu Maadili ya Viongozi wa Umma iliyotolewa na Katibu Msaidizi Kanda ya Kaskazini Bw. Gerald Mwaitebele (hayupo pichani) kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika tarehe 23 Aprili, 2025 katika ukumbi wa Chuo hicho.