Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini-Arusha Bw. Gerald Mwaitebele akiongoza zoezi la upandaji miti katika ziara ya kutembelea klabu za Maadili katika shule ya sekondari ya Mwakoko iliyopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro tarehe 11 Februaru,2025.
Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini-Arusha Bw. Gerald Mwaitebele akiongoza Kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa SP. Ernesta Abel Mwambinga Kamanda wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Babati. Hafla hiyo ilifanyika katika Ofisi ya Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara tarehe 29 Januari,2025.
Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bi. Philipina Kobelo akitoa maelezo ya jinsi ofisi hiyo inavyotekeleza majukumu yake kwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri aliyefika kwenye banda la ofisi hiyo katika Maadhimisho ya Wiki ya Sheria katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2025.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi Bw. Godfrey Mnzava (katikati) akila kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kinachoongozwa na Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini Bw. Gerald A.Mwaitebele (aliyesimama kushoto), haflahiyo ilifanyikakatika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro tarehe 27 Januari, 2025.
Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bi. Philipina Kobelo (mwenye fulana nyekundu) akitoa elimu ya maadili kwa Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza CP. Nicodemus Tenga aliyetembelea banda la ofisi hiyo katika Maadhimisho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma tarehe 29 Januari 2025
Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bi. Philipina Kobelo (mwenye fulana nyekundu) akitoa elimu kwa Mwananchi aliyefika kwenye banda la ofisi hiyo katika Maadhimisho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma tarehe 29 Januari 2025
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Mst) Sivangilwa Mwangesi akifungua mafunzo ya uchunguzi kwa maafisa wachunguzi na watunza kumbukumbu kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Mount Royal Hotel mkoani Iringa tarehe 27 Januari, 2025.
Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati Dodoma Bw. Joshua Mwambande akitoa mada kuhusu maadili kwa waheshimiwa madiwani pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo wa Manispaa ya Singida yaliyofanyika katika ukumbi wa Mwenge Sekondari tarehe 23 Januari, 2025
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida, Mhe. Yagi Maulid akifungua mafunzo ya Maadili kwa waheshimiwa madiwani pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo wa Manispaa ya Singida yaliyofanyika katika ukumbi wa Mwenge Sekondari tarehe 23 Januari, 2025. Mafunzo hayo yameandaliwa na Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati. Kushoto ni Naibu Meya Mhe. Gwae Mbua Na Mkurugenzi wa Manispaa, Bi. Joanfaith Kataraia.
Afisa TEHAMA, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Francis Toke akitoa Mada kuhusu Ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (0nline Declaration System-ODS) katika mafunzo ya Viongozi wa Umma yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara tarehe 17 Desemba 2024.