Baadhi ya washiriki wa mafunzo kuhusu mfumo wa ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (Online Declaration System-ODS) ambao ni Viongozi wa Umma na Maafisa TEHAMA kutoka mkoani Mtwara wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Maadili tarehe 6 Machi, 2026.
Mkuu wa wilaya ya Mtwara, Mhe. Abdallah Mwaipaya akifungua mafunzo ya namna ya ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (ODS). Mafunzo yaliyowashirikisha viongozi wa umma na maafisa TEHAMA kutoka mkoa wa Mtwara yalifanyika katika ukumbi wa Maadili Mtwara tarehe 6 Machi, 2026.
Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Prof. Eliamani Sedoyeka akitoa neno la utangulizi katika kikao kazi cha wawezeshaji wa mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Umma. Kikao hicho kimefanyika tarehe 6 Machi, 2026 jijini Arusha katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA).
Kamishna wa Maadili Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua kikao kazi cha wawezeshaji wa mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Umma. Kikao hicho kimefanyika tarehe 6 Machi, 2026 jijini Arusha katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA).
Baadhi ya washiriki wa mafunzo kuhusu mfumo wa ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (Online Declaration System-ODS) ambao ni Viongozi wa Umma na Maafisa TEHAMA kutoka jiji la Tanga wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Bandari ya Tanga tarehe 05 Machi, 2026.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Mashariki Bw. Hendry Sawe akifungua mafunzo ya namna ya ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (Online Declaration System-ODS) kwa Maafisa TEHAMA kutoka jiji la Tanga. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Bandari ya Tanga tarehe 05 Machi, 2026
Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo vya TEHAMA kutoka Taasisi za Umma na Wizara wakifuatilia mada kuhusu mfumo wa ujazaji Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya Mtandao (Online Declaration System-ODS) katika mafunzo ya maadili yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi jijini Dodoma tarehe 03 Machi, 2026.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati – Dodoma Bw. Anno Mgani akitoa mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa Wakuu wa Idara na Vitengo vya TEHAMA kutoka Taasisi za Umma na Wizara (hawapo pichani) katika mafunzo ya maadili yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi jijini Dodoma tarehe 03 Machi, 2026.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati- Dodoma Bi Jasmin Awadhi akifungua mafunzo ya maadili kwa Wakuu wa Idara na Vitengo vya TEHAMA (hawapo pichani). Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi jijini Dodoma tarehe 03 Machi, 2026.
Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Mashariki – Morogoro Bw. Hendry Sawe akifungua mafunzo ya namna ya ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (ODS). Mafunzo yaliyowashirikisha viongozi wa umma na maafisa TEHAMA kutoka mkoa wa Morogoro yalifanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro tarehe 03 Machi, 2026.