Mkurugenzi wa Tume ya TEHAMA Dkt. Nkundwe Mwasaga akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya mawasiliano ya kidigitali kwa viongozi wa Umma katika mafunzo ya Maadili kwa Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo ya siku tatu yamehitimishwa tarehe 17 April, 2026 katika ukumbi wa Morena mkoani Morogoro.
Bw. Waziri Kipacha Katibu Idara ya Ukuzaji wa Maadili akifungua mafunzo ya wakuu wa Idara na vitengo vya manunuzi na ugavi kutoka Taasisi za umma, mashirika ya umma wakala wa Serikali na mamlaka za Serikali za mitaa kilichofanyika tarehe 16 Aprili, 2026 katika ukumbi wa Hoteli ya SAANAN jijini Dodoma.
Washiriki wa mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Umma ambao ni wakurugenzi wa utawala na rasilimaliwatu wa Wizara, Taasisi na mashirika ya umma (DAHRMs), Makatibu tawala wa Wilaya (Das) wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizowasilishwa. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa hoteli ya Morena mkoani Morogoro tarehe 15 Aprili, 2026.
Mhe. Mathew Kirama, Katibu na Mtendaji Mkuu mstaafu Ofisi ya Rais, Tume ya Utumishi wa Umma akifungua mafunzo ya Maadili kwa Viongozi wa Umma kwa wakurugenzi wa utawala na Rasilimaliwatu wa Wizara, Taasisi na mashirika ya umma (DAHRMs), Makatibu Tawala wa Wilaya (DAS). Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa hoteli ya Morena mkoani Morogoro tarehe 15 Aprili, 2026.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi ambao ni wamiliki, wahariri na waandishi mbalimbali wa habari kutoka mkoani Tanga wakifuatilia mijadala mbalimbali. Kikao kazi hicho kilifanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Bandari mkoani Tanga tarehe 10 Aprili,2026.
Baadhi ya wadau wa habari kutoka mikoa ya Pwani na DaresSalaam walioshiriki Kikao kazi kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika kukuza maadili nchini wakifatilia mada mbali mbali katika kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Shule ya Uongozi Mwalimu Nyerere mjini Kibaha mkoani Pwani tarehe 09 Aprili, 2026.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha ambao ni wahariri na waandishi mbalimbali wa habari kutoka mkoani morogoro wakifuatilia mijadala mbalimbali. Kikao kazi hicho kilifanyika katika ukumbi wa hazina ndogo mkoani Morogoro tarehe 8 Aprili, 2026.
Baadhi ya wadau wa habari wa mikoa ya Kanda ya Kati walioshiriki kikao kazi kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika kukuza maadili nchini wakisikiliza kwa makini hotuba ya ufunguzi katika kikao kazi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Zabibu Hoteli iliyopo jijini Dodoma tarehe 01 April, 2026.
Baadhi ya wadau wa habari walioshiriki Kikao kazi kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika kukuza maadili nchini wakifatilia mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Midland iliyopo Makambako mkoani Njombe tarehe 30 Machi, 2026.
Baadhi ya waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao ni wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakisoma taarifa ya mradi wa jengo la Maadili wakati wa ukaguzi wa mradi huo ulipo wilayani Ilemela mkoani Mwanza. Tukio hilo limefanyika tarehe 15 Machi, 2026.