Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi na Manunuzi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Kenedy Mwakalindile akitoa neno la utangulizi katika kikao kazi cha Maafisa Ununuzi na Ugavi wa ofisi hiyo kilichofanyika tarehe 27 Aprili, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) mkoani Singida
Kamishna wa Maadili Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua kikao kazi cha Maafisa Ununuzi na Ugavi kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kilichofanyika tarehe 27 Aprili, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) mkoani Singida.
Mratibu wa mafunzo ya Maadili na Uadilifu kwa Viongozi wa Umma kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Dkt. Birigitha Ngwano John akitoa neno la ufunguzi katika mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya MORENA mkoani Morogoro tarehe 22 April, 2026.
Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa shule za msingi na sekondari wa Mkoa wa Manyara ambao ni walezi wa klabu za maadili mara baada ya mafunzo ya maadili kwa walimu hao yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.
Baadhi ya walimu kutoka shule za msingi na sekondari mkoani Manyara wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya maadili kwa walimu walezi wa klabu za maadili kutoka shule za Mkoa wa Manyara yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.
Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji akifungua mafunzo ya maadili kwa walimu walezi wa klabu za maadili kutoka shule za mkoani Manyara yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.
Mkurugenzi wa Tume ya TEHAMA Dkt. Nkundwe Mwasaga akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya mawasiliano ya kidigitali kwa viongozi wa Umma katika mafunzo ya Maadili kwa Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo ya siku tatu yamehitimishwa tarehe 17 April, 2026 katika ukumbi wa Morena mkoani Morogoro.
Bw. Waziri Kipacha Katibu Idara ya Ukuzaji wa Maadili akifungua mafunzo ya wakuu wa Idara na vitengo vya manunuzi na ugavi kutoka Taasisi za umma, mashirika ya umma wakala wa Serikali na mamlaka za Serikali za mitaa kilichofanyika tarehe 16 Aprili, 2026 katika ukumbi wa Hoteli ya SAANAN jijini Dodoma.
Washiriki wa mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Umma ambao ni wakurugenzi wa utawala na rasilimaliwatu wa Wizara, Taasisi na mashirika ya umma (DAHRMs), Makatibu tawala wa Wilaya (Das) wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizowasilishwa. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa hoteli ya Morena mkoani Morogoro tarehe 15 Aprili, 2026.
Baadhi ya washiriki wa kikao kazi ambao ni wamiliki, wahariri na waandishi mbalimbali wa habari kutoka mkoani Tanga wakifuatilia mijadala mbalimbali. Kikao kazi hicho kilifanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Bandari mkoani Tanga tarehe 10 Aprili,2026.