Kamishna wa Maadili, Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akisoma taarifa ya mradi wa jengo la Maadili Mwanza kwa wajumbe wa Kamati Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ilipofanya ziara ya ukaguzi wa mradi wa jengo hilo. Tukio hilo limefanyika wilayani Ilemela mkoani Mwanza tarehe 15 Machi, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb) akitoa neno la utangulizi kuhusu mradi wa jengo la Maadili Mwanza kwa wajumbe wa Kamati Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, tukio hilo limefanyika tarehe 15, Machi 2026 wilayani Ilemela mkoani Mwanza.
Baadhi ya waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao ni wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakisoma taarifa ya mradi wa jengo la Maadili wakati wa ukaguzi wa mradi huo ulipo wilayani Ilemela mkoani Mwanza. Tukio hilo limefanyika tarehe 15 Machi, 2026.
Mwenyekiti wa Kamati Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwaongoza wajumbe wa Kamati kukagua mradi wa jengo la utawala la Maadili lililopo wilayani Ilemela mkoani Mwanza, Tukio hilo limefanyika tarehe 15, Machi 2026. Viongozi wengine walioshiriki ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb).
Baadhi ya Watumishi Wanawake kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Makao Makuu na Kanda ya Kati wakiwa katika picha ya pamoja katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Mbande wilayani Kongwa mkoani Dodoma tarehe 8 Machi, 2026.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo kuhusu mfumo wa ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (Online Declaration System-ODS) ambao ni Viongozi wa Umma na Maafisa TEHAMA kutoka mkoani Mtwara wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Maadili tarehe 6 Machi, 2026.
Mkuu wa wilaya ya Mtwara, Mhe. Abdallah Mwaipaya akifungua mafunzo ya namna ya ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (ODS). Mafunzo yaliyowashirikisha viongozi wa umma na maafisa TEHAMA kutoka mkoa wa Mtwara yalifanyika katika ukumbi wa Maadili Mtwara tarehe 6 Machi, 2026.
Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Prof. Eliamani Sedoyeka akitoa neno la utangulizi katika kikao kazi cha wawezeshaji wa mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Umma. Kikao hicho kimefanyika tarehe 6 Machi, 2026 jijini Arusha katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA).
Kamishna wa Maadili Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua kikao kazi cha wawezeshaji wa mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Umma. Kikao hicho kimefanyika tarehe 6 Machi, 2026 jijini Arusha katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA).
Baadhi ya washiriki wa mafunzo kuhusu mfumo wa ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (Online Declaration System-ODS) ambao ni Viongozi wa Umma na Maafisa TEHAMA kutoka jiji la Tanga wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Bandari ya Tanga tarehe 05 Machi, 2026.