Wanafunzi wa sekondari ya Wasichana Nangwa iliyopo wilayani Hanang mkoani Manyara wakifatilia kwa makini mada ya misingi ya maadili kutoka kwa Afisa wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini Bw. Musiba Magoma (hayupo pichani) wakati wa zoezi la kutembelea Klabu za Maadili wilayani humo lililofanyika tarehe 19 Mei, 2026.
Baadhi ya Viongozi kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) walioshiriki mafunzo ya maadili wakifatilia mada mbalimbali katika mafunzo hayo yaliyofanyika tarehe 9 Mei, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Vizano jijini Dodoma.
Dkt. Dotto Bulendu kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine-Mwanza akitoa mada ya utoaji elimu kwa umma kupitia Redio kwa maafisa wa Sekretarieti ya Maadili ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka makao makuu na Kanda wakati wa mafunzo ya kukuza maadili kupitia vyombo vya habari yaliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Flomi mjini Morogoro tarehe 4 Mei, 2026.
Kamishna wa Maadili, Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya kukuza maadili kupitia vyombo vya habari kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma makao makuu na Kanda yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Flomi mjini Morogoro tarehe 4 Mei, 2026.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati. Bi. Jasmin Awadh akitoa mada kuhusu Sheria ya maadili kwa Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma katika mafunzo ya maadili yaliyofanyika ukumbi wa Zabibu Hotel mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma wakifuatilia mada mbalimbali za maadili wakati wa mafunzo ya maadili yaliyofanyika katika ukumbi wa Zabibu Hotel Mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya sheria ya Maadili wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu kutoka katika Wizara na Taasisi mbalimbali za umma. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Zabibu Hotel Mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.
Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa shule za msingi na sekondari wa Mkoa wa Manyara ambao ni walezi wa klabu za maadili mara baada ya mafunzo ya maadili kwa walimu hao yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.
Baadhi ya walimu kutoka shule za msingi na sekondari mkoani Manyara wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya maadili kwa walimu walezi wa klabu za maadili kutoka shule za Mkoa wa Manyara yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.
Katibu Tawala Mkoa wa Manyara Bi. Maryam Ahmed Muhaji akifungua mafunzo ya maadili kwa walimu walezi wa klabu za maadili kutoka shule za mkoani Manyara yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara tarehe 21 Aprili, 2026.