Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretaieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Kanda ya Magharibi-Tabora Bi. Anna Mbasha akifungua mafunzo ya maadili kwa wakuu wa idara na kitengo cha TEHAMA kutoka Halmashauri za Wilaya, Miji na Manispaa kutoka mikoa ya kanda ya Magharibi. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Grand Penta Hotel mkoani Tabora tarehe 12 Februari, 2026.
Katibu msaidizi kanda ya Kaskazini Arusha Bw. Gelard Mwaitebele akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiri wa mafunzo kuhusu mfumo wa ODS yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha tarehe 12 Februari 2026
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya matumizi ya mfumo wa ODS wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi katika mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha tarehe 12 Februari 2026
Katibu Msaidizi Kanda ya Kaskazini Arusha Bw. Gerald Mwaitebele akifungua mafunzo kwa wakuu wa Vitengo vya TEHAMA kuhusu matumizi ya Mfumo wa ODS yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha tarehe 12 Februari 2026.
Katibu Idara ya Ukuzaji Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Waziri Kipacha akitoa mafunzo kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria (hawapo pichani). Mafunzo hayo yamefanyika katika ofisi za Bunge jijini Dodoma tarehe 11 Februari, 2026.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Regina Qwaray (Mb) akitoa neno la utangulizi kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria (hawapo pichani) wakati wa kikao na kamati hiyo kilichofanyika katika ofisi za Bunge jijini Dodoma tarehe 11 Februari, 2026.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kanda ya Kaskazini-Arusha Bw. Josephat Mkumbwa akiwasilisha Mada ya Misingi ya Maadili kwa wanafunzi wa shule ya msingi Dongobesh iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara wakati wa uzinduzi wa klabu ya maadili shuleni hapo tarehe 4 Februari, 2026.
Bw. Alex Manyama Mang’ara, Mkuu wa Kitengo cha Mipango Halmashauri ya wilaya ya Mbogwe akiwa mbele ya Baraza la Maadili kwa tuhuma za kukiuka Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakati akitekeleza majukumu yake. Baraza lilifanya kikao tarehe 14 Januari, 2026 jijini Dodoma katika ukumbi wa Makao Makuu ya Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb) (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma mara baada ya kufanya ziara ofisini hapo tarehe 11 Disemba, 2025. Kulia kwa Waziri Mkuu ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb) na kushoto kwa Waziri Mkuu ni Kamishna wa Maadili Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb) akizungumza na Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma (hawapo pichani) katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo jijini Dodoma tarehe 11 Disemba, 2025 mara baada ya kufanya ziara ofisini hapo.