Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo vya TEHAMA kutoka Taasisi za Umma na Wizara wakifuatilia mada kuhusu mfumo wa ujazaji Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya Mtandao (Online Declaration System-ODS) katika mafunzo ya maadili yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi jijini Dodoma tarehe 03 Machi, 2026.
Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati – Dodoma Bw. Anno Mgani akitoa mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa Wakuu wa Idara na Vitengo vya TEHAMA kutoka Taasisi za Umma na Wizara (hawapo pichani) katika mafunzo ya maadili yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi jijini Dodoma tarehe 03 Machi, 2026.
Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati- Dodoma Bi Jasmin Awadhi akifungua mafunzo ya maadili kwa Wakuu wa Idara na Vitengo vya TEHAMA (hawapo pichani). Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi jijini Dodoma tarehe 03 Machi, 2026.
Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Mashariki – Morogoro Bw. Hendry Sawe akifungua mafunzo ya namna ya ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (ODS). Mafunzo yaliyowashirikisha viongozi wa umma na maafisa TEHAMA kutoka mkoa wa Morogoro yalifanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro tarehe 03 Machi, 2026.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya namna ya ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (ODS) ambao ni viongozi wa umma na maafisa TEHAMA kutoka Halmashauri za mkoa wa Morogoro wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro tarehe 03 Machi, 2026.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya maadili amabao ni waalimu walezi wa klabu za maadili kutoka katika shule zilizopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakifuatilia kwa makini mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo tarehe 27 Februari, 2026.
Afisa Elimu Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Abel Ntupwa akifungua mafunzo ya maadili kwa waalimu walezi wa klabu za maadili (hawapo pichani) kutoka shule mbalimbali za Halmashauri ya Manispaa ya Moshi. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo tarehe 27 Februari, 2026.
Mstahiki Meya wa jiji la Dodoma, Mhe. Alimwoni Chaula akipanda mti wakati wa uzinduzi wa bustani ya maadili iliyopo karibu na Chuo cha Biashara CBE kilichopo jijini Dodoma tarehe 27 Februari 2026. Hafla hiyo imeudhuriwa na wanachama wa Kbalu za Maadili kutoka Chuo cha CBE, Mipango na Chuo Kikuu cha Mtakatifu John.
Kamishna wa Maadili, Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akipanda mti wakati wa uzinduzi wa bustani ya maadili iliyopo karibu na Chuo cha Biashara CBE kilichopo jijini Dodoma tarehe 27 Februari 2026. Hafla hiyo imeudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Dodoma pamoja na wanachama wa Kbalu za Maadili kutoka Chuo cha CBE, Mipango na Chuo Kikuu cha Mtakatifu John.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma, Mhe. Jabir Shekimweri akipanda mti wakati wa uzinduzi wa bustani ya maadili iliyopo karibu na Chuo cha Biashara CBE kilichopo jijini Dodoma tarehe 27 Februari 2026. Hafla hiyo imeudhuriwa na wanachama wa Kbalu za Maadili kutoka Chuo cha CBE, Mipango na Chuo Kikuu cha Mtakatifu John.