Mstahiki Meya wa jiji la Dodoma, Mhe. Alimwoni Chaula akipanda mti wakati wa uzinduzi wa bustani ya maadili iliyopo karibu na Chuo cha Biashara CBE kilichopo jijini Dodoma tarehe 27 Februari 2026. Hafla hiyo imeudhuriwa na wanachama wa Kbalu za Maadili kutoka Chuo cha CBE, Mipango na Chuo Kikuu cha Mtakatifu John.
Kamishna wa Maadili, Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akipanda mti wakati wa uzinduzi wa bustani ya maadili iliyopo karibu na Chuo cha Biashara CBE kilichopo jijini Dodoma tarehe 27 Februari 2026. Hafla hiyo imeudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Dodoma pamoja na wanachama wa Kbalu za Maadili kutoka Chuo cha CBE, Mipango na Chuo Kikuu cha Mtakatifu John.
Mkuu wa wilaya ya Dodoma, Mhe. Jabir Shekimweri akipanda mti wakati wa uzinduzi wa bustani ya maadili iliyopo karibu na Chuo cha Biashara CBE kilichopo jijini Dodoma tarehe 27 Februari 2026. Hafla hiyo imeudhuriwa na wanachama wa Kbalu za Maadili kutoka Chuo cha CBE, Mipango na Chuo Kikuu cha Mtakatifu John.
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Mwanza walioshiriki mafunzo ya maadili wakifuatilia mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 26 Februari, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda akifungua mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Mkoa huo (hawapo pichani). Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza tarehe 26 Februari, 2026.
Baadhi ya Makatibu na Manaibu Makatibu wakuu wa wizara wakifuatilia kwa makini mafunzo ya maadili kwa makatibu na manaibu makatibu wakuu wa Wizara. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Sanaan jijini Dodoma tarehe 20 Februari, 2026.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akitoa neno la utambulisho katika mafunzo ya maadili kwa makatibu na manaibu makatibu wakuu wa Wizara. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Sanaan jijini Dodoma tarehe 20 Februari, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Ikulu (Kazi Maalum) Mhe. Palamagamba Kabudi (Mb) akifungua mafunzo ya maadili kwa makatibu na manaibu makatibu wakuu wa Wizara. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Sanaan jijini Dodoma tarehe 20 Februari, 2026.
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Geita walioshiriki mafunzo ya maadili wakifuatilia mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo yalifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita tarehe 20 Februari, 2026.
Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais, Sekretaieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Kanda ya Ziwa Bw. Godson Kweka akitoa mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa Viongozi wa Mkoa wa Geita (hawapo pichani) katika mafunzo ya maadili yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita tarehe 20 Februari, 2026.