Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deus Clement Sangu (Mb) aliyesimama mbele akipata maelezo kwa namna Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inavyotekeleza majukumu yake, kutoka kwa Afisa wa ofisi hiyo Bi. Desderia Haule (aliyeshika kipaza sauti), alipotembelea banda la ofisi hiyo katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma tarehe 20 Juni, 2025.
Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Kihenzile (Mb) aliyesimama kulia akipata maelezo kuhusu majukumu ya Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka kwa Afisa wa ofisi hiyo Bi. Desderia Haule (wa kwanza kushoto), alipotembelea banda la ofisi hiyo katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma tarehe 19 Juni, 2025.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi akisaini kitabu cha wageni katika banda la Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma tarehe 18 Juni, 2025.
Afisa wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bi. Desderia Haule akitoa maelezo kuhusu Klabu za Maadili kwa walimu wa shule ya msingi Mapambano ya jijini Dar es Salaam waliotembelea banda la ofisi hiyo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma tarehe 18 Juni, 2025
Afisa kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bi. Desderia Haule akielezea majukumu ya ofisi hiyo kwa Dkt. Adolar Duwe ambaye ni Meneja wa Usimamizi wa Rasilimaliwatu na Utawala kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) alipotembelea banda la ofisi hiyo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma tarehe 16 Juni, 2025.
Mwenyekiti wa Baraza la Maadili, Mhe. Jaji (Mst.) Rose Teemba akimkabidhi Tuzo Bw. Peter Ilomo mjumbe wa Baraza la Maadili aliyemaliza muda wake wa kulitumikia Baraza. Tukio hilo limefanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma tarehe 16 Juni, 2025 jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Baraza la Maadili, Mhe. Jaji (Mst.) Rose Teemba (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza pamoja na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma jijini Dodoma tarehe 16 Juni, 2025. Kushoto kwake ni Bi. Suzan Mlawi (mjumbe wa Baraza) na kulia kwake ni Bw. Peter Ilomo anayemaliza muda wake wa kulitumikia Baraza la Maadili.
Wahariri wa vyombo mbalimbali vya Habari nchini wakifuatilia Elimu ya Maadili inayotolewa na Katibu Msaidizi Idara ya Ukuzaji Bw. Fabian Pokela (Hayupo pichani) kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa mkutano wa Wahariri uliofanyika tarehe 30 Mei, 2025 jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi akifungua mkutano wa Wahariri wa vyombo mbalimbali vya Habari nchini uliofanyika tarehe 30 Mei, 2025 jijini Dar es Salaam.
Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Fabian Pokela hayupo pichani, akiongoza kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa baadhi ya Viongozi kutoka katika Taasisi mbali mbali nchini mara baada ya mafunzo ya Maadili yaliyofanyika katika ukumbi wa Golden Crest Hotel iliyopo Jijini Arusha tarehe 14 Mei,2025.