JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

PO-ETHICS SECRETARIAT Logo
DC Mwaipaya: Tusisubili hadi tuitwe na Maadili
06 Mar, 2026
DC Mwaipaya: Tusisubili hadi tuitwe na Maadili

Mkuu wa wilaya ya Mtwara, Mhe. Abdallah Mwaipaya ametoa wito kwa viongozi wa umma nchini kuondokana na tabia ya kusubiri hadi waitwe na Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ndio waanze kujaza Tamko la Rasilimali na Madeni.

Wito huo ameutoa wakati akifungua mafunzo ya ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (Online Declaration System - ODS) yaliyotolewa kwa viongozi wa umma mkoani Mtwara tarehe 6 Machi, 2026 katika ukumbi wa Maadili Mtwara.

Mhe. Mwaipaya amesema kuwa Viongozi wa Umma wanatakiwa kuwasiliana na Sekretarieti ya Maadili mapema pale ambapo watapata changamoto hili iweze kutatuliwa mapema na kuepuka kuitwa na kwa kosa la kushindwa kujaza Tamko la Rasilimali na Madeni.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa wilaya, kama hujaitwa usije kudhani unajaza ni gelesha tu kwa kuwa kila mwaka una jaza na hujawai kuitwa na kuona kama wanakusumbua tu ila tambua Sekretarieti ya Maadili wakati wowote wanaweza kukuita na kutaka utoe maelezo kuhusu Tamko lako, hivyo ni wajibu wetu sote kama viongozi kuepuka adhaa ya kujaza rasilimali kwa mazoea.

 “Kuna siku utaitwa kwa kosa tu la kushindwa kujaza Tamko la Rasilimali na Madeni  kwa uzembe wako au kwa kuwa ulichukulia poa kwa kuwa kila mwaka unajaza ila siku utapoacha kujaza ndio siku utaitwa na kutakiwa kueleza,alisema Mhe. Mwaipaya.

Kaimu Katibu Msaidizi Kanda ya Kusini - Mtwara Bw. Ramadhan Ramadhan aliwaambia viongozi kuwa dirisha la kujaza Tamko la Rasilimali na Madeni la mwaka linafunguliwaga mapema kuanzia tarehe 1 Oktoba hadi 31 Disemba kila mwaka, hivyo ni wajibu kwa viongozi kuanza kujaza mapema pale dirisha linapokuwa wazi.

Afisa Maadili kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Ramadhan Ng’wanang’waka alitoa mafunzo kwa viongozi hao namna ya kujaza Tamko kwa njia ya mtandao.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >