JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

PO-ETHICS SECRETARIAT Logo
Weledi, maarifa na jitihada vyatajwa katika kufanikisha malengo ya Taasisi na Taifa
18 Mar, 2026
Weledi, maarifa na jitihada vyatajwa katika kufanikisha malengo ya Taasisi na Taifa

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wametakiwa kufanya kazi kwa weledi, maarifa na jitihada katika kufikia malengo ya Taasisi na Taifa kwa ujumla.

Rai hiyo imetolewa na Kamishna wa Maadili nchini Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi wakati akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo makao makuu jijini Dodoma tarehe 18 Machi, 2026.

“Kila mtumishi kwa nafasi yake atekeleze majukumu yake  kwa weledi, maarifa, jitihada na mapenzi, huku akitambua kuwa anategemewa kwa nafasi aliyonayo na kwamba yeye ni kipande au kiungo katika mkufu kwenye suala la kuleta maendeleo ya Taasisi na Taifa kwa ujumla,” alisema Mhe. Mwangesi.

Aidha Jaji Mwangesi ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha watumishi wa ofisi hiyo kuendelea  kufanya kazi kwa bidii na kwa kushirikiana huku wakizingatia utunzaji siri za Serikali wanazozipata wakati wakitekeleza majukumu yao.

“Katika kufanikisha malengo ya Taasisi yetu na Taifa, suala la ushirikiano baina yetu halina mbadala hivyo ninaomba ushiriki wa kila mmoja katika kufanikisha malengo ya Taasisi na kujitaidi katika kutunza siri za Serikali,” alisisitiza Mhe. Mwangesi.

Mhe. Mwangesi ameongeza kuwa Katika kuendelea kutekeleza majukumu hayo ni vyema kila mtumishi wa ofisi hiyo kutambua kuwa wamepewa dhamana ya kuiwezesha Serikali kutekeleza majukumu yake na kukumbuka kuwa  Taasisi hiyo ndiyo taswira ya Taifa linapokuja suala la uadilifu.

“Ninaomba sote tufahamu kuwa katika utekelezaji wa majukumu yetu tunapokea maelekezo kutoka maeneo tofauti ambayo tunapaswa kuyatekeleza kwa mujibu wa sheria, kanuni, taratibu na weledi na kwa kuwa tumeajiriwa ili tufanye kazi hivyo tuache uzembe, uvivu na mazoea na tuepuke kuwa chanzo au sababu ya kuikwamisha Serikali katika utendaji wake,” aliongeza Mhe. Mwangesi.

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >