JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Mamlaka na Majukumu

 

           Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ina mamlaka na majukumu yafuatayo:-

  • Kupokea taarifa za mali na madeni zinazohitajika kutolewa na  Viongozi wa Umma kwa mujibu wa Sheria;
  • Kupokea malalamiko na tuhuma kuhusu ukiukwaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoka kwa wanachi;
  • Kufanya uchunguzi wa awali wa tuhuma au malalamiko dhidi ya kiongozi yoyote wa umma anayetuhumiwa kuvunja masharti ya Sheria ya Maadili ya Viongozi;
  • Kuanzisha na kufanya uchunguzi wowote kuhusu ukiukwaji wa Maadili yaliyotajwa katika Sheria bila kusubiri malalamiko kutoka kwa Wananchi;
  • Kuhakiki taarifa za Rasilimali na Madeni zinazotolewa na Viongozi wa Umma kwa mujibu wa Sheria;
  • Kuwaelimisha Viongozi wa Umma na Wananchi kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma pamoja na kazi za Sekretarieti;
  • Kutunza daftari la Rasilimali , Maslahi na Madeni ya Viongozi wa Umma;
  • Kuratibu na kuwezesha shughulli za Baraza la Maadili;
  • Kuwasilisha kwa Rais mapendekezo ya Baraza la  Maadili kuhusu uchunguzi wa kina wa tuhuma za ukiukwaji wa maadili dhidi ya Viongozi wa Umma;
  • Kufanya utafiti juu ya uzingatiaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
  • Kumtaka mtu yoyote kufika mbele ya Sekretarieti ya Maadili kwa ajili ya mahojiano ambayo yatasaidia katika uchunguzi wa ukiukwaji wa maadili;
  • Kukagua akaunti ya Benki ya Kiongozi yoyote wa Umma kwa idhini ya Mahakama pale ambapo Sekretarieti inatarajia kufanya uchunguzi dhidi ya kiongozi husika;
  • Kumtaka Kiongozi anayetuhumiwa kwa kutoa tamko la uongo la rasilimali zake kuthibitisha au kurekebisha Tamko lake;
  • Kutoa idhini ya kukagua Daftari la Raslimali, Maslahi na Madeni ya Kiongozi wa Umma kwa Mwananchi aliyekidhi vigezo;
  • Kumtaka mtu yoyote kuwasilisha kitabu, nyaraka au nakala iliyothibitishwa au kielelezo chochote ambacho kitasaidia uchunguzi kuhusu ukiukwaji wa Maadili.

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >