JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

WATUMISHI BODI YA TUMBAKU WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU SHERIA YA MAADILI
14 Aug, 2025
WATUMISHI BODI YA TUMBAKU WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU SHERIA YA MAADILI

Watumishi wa Bodi ya Tumbaku Tanzania (TTB) wamepatiwa mafunzo kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na kutakiwa kufanya kazi kwa pamoja, kuzingatia uadlifu na nidhamu ili kutimiza malengo ya Taasisi yao.

Wito huo umetolewa na Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Fabian Pokela katika mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Nyerere uliopo katika hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza Agosti 14, 2025.

Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uwezo watumishi wa Bodi ya Tumbaku nchini  kutekeleza majukumu kwa kuzingatia viwango vya juu vya uadilifu, nidhamu na kutoa huduma bila upendeleo kwa kila mmoja.

“Uadilifu katika kutekeleza majukumu yetu ni chachu ya maendeleo kwa jamii yoyote ile, takriban nchi zote zilizofanikiwa, zimekuwa na viwango vya juu vya uadilifu katika kutimiza malengo yao,’’ alisema Bw. Pokela.

Aidha, Bw. Pokela amesisitiza kuzingatia utoaji bora wa huduma na muonekano mzima wa mtoa huduma kwa kuzingatia kanuni zilizowekwa ili kuepuka upendeleo na kutoa huduma chini ya kiwango ama kwa upendeleo.

“Katika kutoa huduma lazima tuzingatie huduma yenyewe, namna huduma inavyotolewa na unadhifu wa mtoa huduma mwenyewe. Mtoa huduma anatakiwa kuvaa kulingana na waraka wa mavazi wa mtumishi wa Umma, vigezo hivi lazima vizingatiwe kwa mtoa huduma yoyote ambaye ni mtumishi wa umma,’’ alisisitiza.

Awali akifungua mafunzo hayo Mkurugenzi Mkuu wa TTB Bw. Stanley Mnozya alisema kuwa wao kama Bodi wameandaa mafunzo hayo kwa lengo la kuwakumbusha watumishi misingi ya maadili katika utumishi wa umma kwani ndio ufunguo katika kutekeleza majukumu ya kila siku.

“Tutahakikisha kila mwaka tunaandaa mafunzo ya namna hii kwa watumishi wetu maana mtumishi mwema lazima awe na maadili mema na kujali rasilimali za nchi kwanza kwa maendeleo ya Taasisi na Taifa kwa ujumla,” alisema Bw. Mnozya.

Mafunzo hayo  ya siku mbili pia yana wakumbusha watumishi kuzingatia uadilifu, kuepuka vitendo vya kutoa na kupokea rushwa, nidhamu na kujali afya wakati wa utekelezaji wa majukumu yao. Jumla ya watumishi 73 wameshirikii mafunzo hayo.

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >