JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Sekretarieti ya Maadili yafungua Klabu mpya 20 za maadili wilayani Kongwa
16 May, 2025
Sekretarieti ya Maadili yafungua Klabu mpya 20 za maadili  wilayani Kongwa

Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati-Dodoma imeanzisha klabu mpya 20 za maadili kwa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri ya  Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma.

Akiongoza zoezi la kuanzisha klabu hizo kati ya tarehe 13 hadi 15 Mei, 2025 Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya kati Bi. Jasmin Awadhi amesema kuwa wamefanikisha  kuzindua klabu hizo kwa ushirikiano mkubwa na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya  hiyo  Dkt. Omary Nkullo.

‘’Lengo letu ilikua kufungua klabu 20 za maadili kwa Kata nne za Wilaya ya Kongwa ambazo ni Kata ya Kongwa, Ugogoni, Sejeli pamoja na Hogoro na mpaka tunavyoongea hapa ni kuwa  tumefanikiwa kutimiza lengo hilo kwa kufungua idadi hiyo ya klabu 20 tulizojiwekea katika malengo yetu,’’ alisema Bi. Jasmin.

Bi. Jasmin ameongeza kuwa licha ya kufungua klabu hizo mpya 20 pia wamefanikiwa kuitembelea na kuhuisha klabu moja ya zamani iliyopo katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) wilayani humo na kuongeza kuwa wanaushukuru uongozi wa Wilaya ya Kongwa kwa kuwa bega kwa bega katika kufanikisha zoezi hilo ambalo ni endelevu.

Kati ya shule hizo 20 zilifanikiwa kupata klabu za maadili, shule za msingi ni 16 na shule nne ni za sekondari ambapo zipo katika kata hizo nne zilizofikiwa katika  zoezi hilo ambapo takribani kila uongozi wa shule zote hizo umelipokea zoezi hilo kwa mikono miwili na kulifurahia kwa namna tofauti.

Shule za msingi zilizofanya uzinduzi wa klabu hizo ni Ubalozi, Viganga, Mlanga,Ibwaga, Padre Corado, Mnyakongo, Nguji, Mautya, Machenje, Sejeli, Msunjilile, Banyibanyi, Mkutani, chilingo, Tumaini pamoja na shule ya msingi Job Ndugai.

Kwa upande wa shule za sekondari zilizopata klabu za maadili ni pamoja na Msunjilile, Banyibanyi, Mnyakongo na Ibwaga.

Akizungumza mara baada ya kufunguliwa kwa klabu ya Maadili shuleni kwake, Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Tumaini Bw. Mussa Samweli Joseph ameipongeza  Sekretarieti ya Maadili na kuishukuru kwa kuichagua shule yao kuwa miongoni mwa shule zilipata klabu za maadili wilayani humo na kuahidi kutoa ushirikiano katika kuiendeleza klabu hiyo.

 ‘’Kwanza niwapongeze na kuwashukuru kwa hatua hii na pia niwaombe muendelee kuwa na sisi pamoja na klabu nyingine mnazozisimamia ,kwani kwa namna hii itasaidia kupata Viongozi waadilifu na pia Raia wema na wazuri kwa kizazi cha baadae,’’ alisema Bw. Mussa.

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >