JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

PO-ETHICS SECRETARIAT Logo
Wawezeshaji wa mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Umma watakiwa kuwa mabalozi wa mabadiliko ya maadili
06 Mar, 2026
Wawezeshaji wa mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Umma watakiwa kuwa mabalozi wa mabadiliko ya maadili

Wawezeshaji wa mafunzo ya Maadili kwa Viongozi wa Umma wametakiwa kuwa mabalozi wa mabadiliko ya maadili katika utumishi wa umma.

Kauli hiyo imetolewa na Kamishna wa Maadili nchini Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi wakati akifungua kikao kazi cha wawezeshaji wa mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Umma kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) jijini Arusha tarehe 6 Machi. 2026.

“Ushiriki wenu katika hili sio wa bahati mbaya, unaonyesha imani ambayo Taasisi hizi mbili zimeweka kwenu kutokana na utaalamu wenu pamoja na uwezo wenu wa kufundisha, kuhamasisha na kusimamia viwango vya juu vya maadili, hivyo ninyi sio wawezeshaji tu, bali pia ni mabalozi wa mabadiliko ya maadili katika utumishi wa umma,” alisema Mhe. Mwangesi.

Aidha Mhe. Mwangesi ameongeza kuwa wao kama wawezeshaji wa mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Umma kupitia wao Viongozi wa Umma wataweza kupata maarifa, misingi na miongozo ya maadili na hatimaye kujenga mfumo wa uongozi unaozingatia uwajibikaji, haki na uadilifu kwa manufaa ya Taifa.

“Kupitia ninyi Viongozi wa Umma wataweza kupata maarifa mbali mbali kuhusu maadili ,hivyo nawaomba kuongeza ubunifu katika mbinu mnazotumia katika kufundishia,” alisisitiza.

Awali akitoa neno la utangulizi Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Prof. Eliamani Sedoyeka amesema kuwa lengo la kikao kazi hicho ni kupitia na kuboresha mpango kazi wa utoaji wa elimu ya maadili kwa Viongozi wa Umma ambao ulianza mwaka jana kwa ushirikiano kati ya Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

“Ni fursa nzuri kufanya kazi na Taasisi yenye jukumu nyeti la kusimamia maadili ya Viongozi wa Umma nchini, hivyo tupo hapa kupitia na kuangalia changamoto tulizopata katika awamu ya kwanza ambayo imemalizika vizuri licha ya changamoto za hapa na pale, na kisha kuboresha penye mapungufu,”alisema Prof. Sedoyeka.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu kutoka Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Dkt. Grace Idinga amesema kuwa licha ya changomoto za hapa na pale walizopata katika awamu ya kwanza bado Viongozi walijitokeza kushiriki mafunzo hayo na wanatajia Viongozi  wengi zaidi watajitokeza katika mafunzo ya awamu ya pili yanayotajiwa kuanza baadae mwezi huu.

“Viongozi 204 walijitokeza kushiriki katika awamu ya kwanza ya mafunzo haya, sawa na 24% ya malengo yetu,hivyo ni matarajio yetu awamu ya pili tutapata Viongozi wengi zaidi na pia tutafanyia kazi changamoto za awamu ya kwanza.” alisema Dkt. Grace.

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >