JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

PO-ETHICS SECRETARIAT Logo
Wawakilishi wa vyombo vya habari nchini Kanda ya Kusini Mtwara wapigwa msasa kuhusu Maadili
10 Apr, 2026
Wawakilishi wa  vyombo vya habari nchini Kanda ya Kusini Mtwara wapigwa msasa kuhusu Maadili

Vyombo vya habari nchini vimetakiwa kuhakikisha vinatoa mchango mkubwa katika  kuimarisha na kukuza maadili ya viongozi  wa Umma nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kanda ya kusini Mtwara Bw. Manula alipokuwa akifungua kikao kazi na wawakilishi wa vyombo vya habari kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Rais Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi Kanda ya kusini Mtwara tarehe 10 mwezi April 2026.

Aidha Bw Manula katika hotuba yake amesisitiza ushiriano mzuri kati ya Sekretarieti na vyombo vya habari nchini kuhakikisha Maadili ya viongozi yanaimarika  kupitia vyombo vya habari nchini.

Ameongeza kuwa  ushirikiano kati ya Sekretarieti ya Maadili na vyombo vya habari utasaidia kupanua uwigo na kujenga imani ya wanachi na Sekretarieti pamoja wananchi kwa ujumla.

Bw. Manula ametoa wito kwa wawakilishi wa vyombo hivyo vya habari wanakuwa mabalozi wazuri katika kuhakikisha kuwa Maadili yanakuzwa na kuimarika kwa kutoa Elimu ya Maadili kupitia vyombo mbalimbali vya habari nchini

Akitoa neno la ufunguzi Mkurugenzi wa mipango na ufatiliaji Bw. Omary Juma amewataka wawakilishi wa vyombo vya habari nchini kuhakikisha ushirikiano uliopo kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na vyombo vya habari katika kanda ya kusini Mtwara  unaimarika katika kusimamia na kukuza maadili kwa  kuelimisha umma na wananchi kupitia vyombo vya habari.

Akitoa mada kuhusu majukumu ya Sekretarieti ya Maadili Afisa Maadili kanda ya kusini Mtwara Bw. Yusuph Sumbu ametaja baadhi ya majukumu ya Sekretarieti ya Maadili ya viongozi wa Umma kuwa ni pamoja na  kupokea Matamko ya Raslimali na madeni ya viongozi wa Umma, kutoa Elimu ya Maadili kwa viongozi na wananchi pamoja na kupokea malalamiko dhidi ya viongozi wanaokiuka maadili kutoka kwa  wanachi na kuanzisha kufanya uchunguzi wa kina kuhusianana malalamiko hayo.

Kikao kazi hicho cha siku moja kilikuwa na lengo la kuhakikisha ushirikiano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na vyombo vya habari unaimarika katika kuhakikisha kuwa uwajibikaji wa viongozi unaongezeka kupitia vyombo vya habari nchini.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >