JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Watumishi wapya Sekretarieti ya Maadili watakiwa kufanya kazi kwa bidii na kwa Uadilifu mkubwa
06 Oct, 2025
Watumishi wapya  Sekretarieti ya Maadili watakiwa kufanya kazi  kwa bidii na kwa Uadilifu mkubwa

Watumishi wapya walioajiriwa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wametakiwa kuwa wabunifu, kufanya kazi kwa bidii, kuzingatia ushirikiano ili kutimiza malengo ya Taasisi na Serikali kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi alipokuwa akifungua mafunzo kwa watumishi hao yaliyofanyika tarehe 6 Oktoba, 2025 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo Makao Makuu Dodoma.

‘’Mkiwa kama watumishi wapya, mna jukumu muhimu la kutoa mawazo mapya  hata kama ni madogo yanaweza kuwa na tija katika kuleta mafanikio ya pamoja na yote haya yatafanyika kama mtafanya kazi kwa bidii na ushirikiano katika kutekeleza majukumu yenu.’’ Alisema Mhe. Mwangesi.

Mhe. Jaji (Stahiki) Mwangesi katika hotuba yake  amebainisha kuwa  mafunzo  hayo ni  nguzo  kuu kwa Watumishi hao  katika kufanya kazi   kwa bidii na kwa uadilifu mkubwa katika  Utumishi wa Umma.

‘’Kila mmoja wenu anatakiwa kuzingatia mafunzo haya ,kwani ndio msingi katika Utumishi wa Umma na utakupelekea kufanya kazi kwa ufanisi na kwa viwango vilivyokusudiwa hadi utakapohitimisha Utumishi wako.’’ Alisisitiza

Awali akitoa neno la utangulizi Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bi. Teddy Njau amesema kuwa mafunzo hayo ya siku tatu yanalenga  kuwafanya  Watumishi hao kujua Kanuni na Sheria za Utumishi wa Umma katika kutekeleza majukumu yao.

“Mafunzo haya ni muhimu kwenu katika kufanya kazi na ni matumaini yangu baada ya mafunzo hayo kila mmoja wetu atakua amepata kitu na hatimaye kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na Sheria zilizopo katika utumishi wa Umma.’’ alisema.

Mafunzo haya ya siku tatu yamewashirikisha watumishi wapya kutoka katika ofisi zote za kanda pamoja na Makao Makuu.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >