JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Watumishi wa Umma watakiwa kukemea vitendo vya ufunjifu wa Haki za Binadamu.
10 Dec, 2024
Watumishi wa Umma watakiwa kukemea vitendo vya ufunjifu wa Haki za Binadamu.

Watumishi wa Umma wametakiwa  kukemea vitendo vya ukiukwaji wa Maadili, Rushwa  na  uvunjifu  wa Haki za Binadamu wanapotekeleza majukumu yao ili kuleta ufanisi katika  kutoa huduma bora kwa  wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu Mhe Jaji (Stahiki) Mathew Mwaimu katika kongamano la kilele cha maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu lililofanyika jijini Dodoma katika Ukumbi wa PSSSF tarehe 10 Desemba 2024.

“Lengo kuu la kongamano hili ni kutoa fursa kwa watumishi wa Umma kujitathimini namna wanavyotoa huduma kwa wananchi kwa kuzingatia  Maadili na Haki za Binadamu na jinsi wanavyoweza kuepuka vitendo vya Rushwa wanapotekeleza majukumu yao “alisema.

Aidha Mhe, Mwaimu amewaasa watumishi wa Umma kutumia kongamano hili pamoja na mada zitakazotolewa kuepuka vitendo sivivyo vya kimaadili na vya ukiukwaji wa Haki za Binadamu wanapotoa huduma kwa wananchi ambavyo ni pamoja na Rushwa, unyanyasaji, dharau, kejeli na maringo na kwamba havitakiwi katika utumishi wa Umma.

Mhe. (Jaji) Mwaimu katika hotuba yake pia aliwataka viongozi wa Umma kufanyia kazi malalamiko yaliyotolewa na wananchi wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa wa 2024 ili yasijirudie katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2025.

Mhe Mwaimu amefafanua kuwa vitendo vya uvunjifu wa Amani kwa wananchi pamoja na ukiukwaji wa Haki za Binadamu ni kosa kubwa na kwamba halitakiwi kufumbiwa macho.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni Tumia haki yako ya kidemokrasia chagua Viongozi waadilifu na wanaozingatia haki za binadamu na misingi ya utawala bora kwa maendeleo ya Taifa.

Mada mbili zimewasilishwa na kujadiliwa katika kongamano hilo ambazo ni Haki za binadamu katika mapambano dhidi ya Rushwa na mada ya pili niMaadili, Haki na  wajibu wa watumishi wa Umma.

Maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu kitaifa yameratibiwa na Taasisi zinazosimamia Utawala Bora nchini ambazo ni Ofisi ya Rais Ikulu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Sekretarieti ya Maadili ya  Viongozi wa Umma, Wizara ya Katiba na Sheria, Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa, Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Tume ya Utumishi wa Umma, Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali pamoja na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.

 

 

 

 

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >