JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Watumishi wa TRA- Arusha waaswa kuzingatia Ahadi ya Uadilifu
27 Oct, 2023
Watumishi wa TRA- Arusha waaswa kuzingatia Ahadi ya Uadilifu

Watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoani Arusha wametakiwa kuzingatia masharti ya Ahadi ya Uadilifu katika utendaji kazi wao wa kila siku.

Hayo yalisemwa na Afisa wa Maadili kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini-Arusha Bw. Tumaini Mgalla i wakati akitoa mada kuhusu Ahadi ya Uadilifu kwa watumishi haohivi karibuni .

Bw. Mgalla alieleza kuwa Hati ya Ahadi ya Uadilifu ni tamko rasmi la kimaandishi linalotolewa na Viongozi wa Umma pindi wanapoteuliwa au kuchaguliwa kuonyesha dhamira ya kuzingatia misingi ya maadili na mapambano dhidi ya rushwa.

Katika mada yake Bw.Mgalla alizitaja athari za kukiuka masharti ya Ahadi ya Uadilifu kuwa ni pamoja na kiongozi wa umma kuchukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria, wananchi kutokuwa na imani na serikali yao.

“Kiongozi wa Umma asipoyaishi yale aliyoahidi katika kiapo chake ni dhahiri kuwa wananchi watakosa imani na kiongozi huyo pamoja na Serikali kwa ujumla,” alisema.

Aidha Bw. Mgalla alifayataja baadhi ya masharti yaliyopo katika Hati ya Ahadi ya Uadilifukuwa ni pamoja na;Uwazi katika utekelezaji wa shughuli za umma na kufanya maamuzi; Uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu ya umma;Uadilifu katika utendaji wa kazi za umma naKuzingatia weledi katika utendaji kazi za umma.

Masharti mengine ni; Uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu; Uzalendo kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;Uaminifu katika shughuli za umma ili kulinda fedha na mali nyinginezo za umma;Kuepuka mgongano wa maslahi, Matumizi sahihi ya taarifa na Kutoa huduma bora bila upendeleo.

“Baada ya kiongozi wa umma kusaini hati hiyo, anawajibika kutekeleza masharti yote yaliyoko katika Hati ya Ahadi ya Uadilifu ili kuleta uwazi katika utendaji wake wa kazi na wananchi kuwa na imani na Serikali yao,” alisema.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >