JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

WATUMISHI WA SEKRETARIETI YA MAADILI WATAKIWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA WELEDI NA UADILIFU.
27 Oct, 2023
WATUMISHI WA SEKRETARIETI YA MAADILI WATAKIWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA WELEDI NA UADILIFU.

Watumishi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa weledi na uadilifu wa kiwango cha juu kwa maslahi mapanaya taifa letu.

Kauli hiyo imetolewana Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi katika kikao cha baraza la wafanyakazi wa Sekretarieti ya Maadili kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) tarehe 24 Agosti,2023.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Mhe. Mwangesi alisema kuwa katika kutekeleza majukumu ya Taasisi watumishi wanatakiwa kuacha uzembe, uvivu na kuepuka kufanya kazi kwa mazoea ili kujenga imani kwa wananachi na Serikali iliyopo madarakani na kwamba wasiwe chanzo au sababu ya kukwamisha utekelezaji wa majukumu.

“Kila mtumishi kwa nafasi yake anatakiwa kuacha uzembe na kufanya kazi kwa weledi na kutambua kuwa ana wajibu wa kukuza maadili” amesema na kuongeza kuwa watumishi wa Sekretarieti ya Maadili wafanye kazi kwa bidii na kutunza siri za Serikali.

Aidha, Mhe. Mwangesiameeleza kuwa changamotozinazoikabilitaasisi zimepungua kwa kiasi kikubwa ikiwemo uhaba wa majengo ya ofisi zinazomilikiwa na taasisi, ambapo kwa sasa Ofisi inategemea kukamilisha baadhi ya majengo yake katika mwaka huu wa fedha.

Awali akitoa neno la ukaribisho katika kikao hicho Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Bi.Teddy Njau alieleza kuwa kikao hicho ni kwa mujibu wa Waraka wa Rais , Na. 1 wa mwaka 1971 unaoelekeza kila Taasisi kuwa na Baraza la Wafanyakazi

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >