JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

WATUMISHI WA SEKRETARIETI YA MAADILI WAMETAKIWA KUTUMIA TEKNOLOJIA KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO.
22 Mar, 2024
WATUMISHI WA SEKRETARIETI YA MAADILI  WAMETAKIWA KUTUMIA TEKNOLOJIA KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO.

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa weledi unaoendana na matumizi ya teknolojia kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Miongozo mbalimbali kuongeza  ufanisi katika  utekelezaji wa majukumu yao.

Kamishna wa Maadili, Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi alitoa agizo hilo alipokuwa akifungua kikao cha Baraza la wafanyakazi kilichofanyika katika ukumbi wa Ngorongoro jijini Arusha tarehe 20 Machi 2024.

“Fanyeni kazi kwa weledi na ubunifu unaoendana na kasi ya teknolojia na maendeleo ya Dunia huku mkizingatia sheria, kanuni na miongozo mbalimbali inayotolewa na viongozi wenu.” alisema,

 

Aidha, Mhe. Mwangesi katika hotuba yake ya ufunguzi aliwataka wajumbe wa Baraza la wafanyakazi kushiriki kikamilifu katika kujadili na kujipima utendaji wao wa kazi ili kuendelea kutoa huduma bora kwa uwazi, ufanisi na tija inayokidhi maslahi mapana ya Watanzania na Taifa kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Mhe. Mwangesi alieleza kuwa Sekretarieti ya Maadili imefanya kikao hicho cha Baraza la wafanyakazi ili kuzingatia agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  la mwaka 1970 na ni utekelezaji wa kifungu cha 73(1-3) cha sheria Na. 6 ya mwaka 2004 ya ajira na mahusiano kazini kinachoelekeza kutekeleza sera ya ushirikishwaji wa wafanyakazi katika uamuzi wa pamoja

“Baraza la Wafanyakazi ndilo jukwaa la kisheria la majadiliano ya pamoja, kati ya menejimenti na watumishi mahala pa kazi kujadili masuala mbalimbali yanayowahusu wafanyakazi na waajiri wao, kwa lengo la kuhakikisha waajiri na watumishi wanatambua wajibu na haki zao, kuzingatia Sheria, Kanuni na maadili ya utumishi wa Umma kuleta matokeo chanya ya utendaji kazi wenye tija kwa taasisi na Taifa kwa ujumla,” alisema.

Kwa upande wake Katibu wa TUGHE mkoa wa Dodoma Bw. Samwel Nyungwa alisema, vyama vya wafanyakazi sio adui dhidi ya timu ya Menejimenti ila vipo kwa ajili ya kutoa ushirikiano mzuri kati ya wafanyakazi na uongozi, kitu ambacho sisi TUGHE tumefuraishwa na jinsi tawi letu la Sekretarieti ya maadili ya Viongizi wa Umma linavyopata ushirikiano na tunaomba ushirikiano huu uendelee.

Mwenyekiti wa tawi la TUGHE, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bw. Mahina Henjewele aliupongeza uongozi wa Taasisi kwa kutoa uhuru pale shughuli za tawi zinapofanyika na kuhitaji msaada wa mwajiri.

“Naomba kutoa shukrani kwa uongozi wa Taasisi ambao wakati wote umekuwa ukitoa ushirikiano wa kufanikisha shughuli za tawi,” alisema.

Kikao hicho cha Baraza la wafanyakazi kiliwashirikisha viongozi kutoka makao makuu ya chama cha wafanyakazi (TUGHE) Taifa, Mkoa na wajumbe kutoka katika ofisi za Kanda na makao makuu.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >