JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Watumishi wa Sekretarieti ya Maadili waadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma Kitaifa kwa kupanda miti.
27 Oct, 2023
Watumishi wa Sekretarieti ya Maadili waadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma Kitaifa kwa kupanda miti.

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini - Arusha wameadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma kwa kupanda miti katika shule ya Msingi Kijenge iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Arusha, mkoani Arusha mapema wiki hii

Watumishi hao wamepanda miti mbalimbali katika maeneo ya shule ya msingi Kijenge kwa kushirikiana na baadhi ya wanafunzi wa Klabu ya Maadili ya shule hiyo.

Akizungumza na wanafunzi hao, Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini Bi. Anna Mbasha aliwaasa wanafunzi kuwa waadilifu, na mfano wa kuigwa kwa kuwa na tabia njema.

“Nyinyi ni taifa la kesho, hivyo, mnatakiwa kujiepusha na vitendo vya utovu wa maadili kama kuchukua vitu vya wenzenu bila kuomba na msome kwa bidii ili muweze kufanya vizuri katika masomo yenu,” alisema.

Bi. Anna alitoa rai kwa wanafunzi hao kuhakikisha miti iliyopandwa inatunzwa vizuri ili baadaye wanufaike na matunda yake ambayo ni matunda, kivuli na usafi wa mazingira ya shule yao.

Awali akimkaribisha Katibu Msaidizi, Mwalimu Mlezi wa Klabu ya maadili shuleni hapo Bw. Mosses Mhando aliishukuru Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini kwa kufungua klabu ya Maadili katika shule ya Kijenge na kupanda miti mbalimbali katika eneo la shule lililotengwa kwa ajili ya Klabu ya Maadili.

“Tutahakikisha miti hii tuliyoipanda leo, yote inatunzwa vizuri na hatimaye itawasaidia wanafunzi kufaidi matunda yatakayotokana na miti hii ikiwemo kivuli, kupendezesha eneo la shule na kuhifadhi mazingira ya shule.” Alisema Bw.Mosses.

Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Kitaifa yalianza tangu Juni 16, 2022 na kilele chake ni hadi Juni 23, 2022.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >