JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Watumishi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji ( EWURA) watakiwa kuzingatia misingi ya maadili.
27 Oct, 2023
Watumishi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji ( EWURA) watakiwa kuzingatia misingi ya maadili.

Watumishi wa Mamlaka ya Udhibiti wa huduma za Nishati na Maji ( EWURA ) wametakiwa kuzingatia misingi ya Maadili katika sekta ya Umma ili kulinda maslahi ya Umma na kukuza Uwajibikaji kwa umma katika utekelezaji wa Majukumu yao ya kila siku.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Msaidizi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati- Dodoma Bi Jasmin Awadh katika mafunzo kuhusu maadili kwa watumishi hao.

Bi. Jasmin alifafanua kuwa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Sheria ya Utumishi wa Umma pamoja na kanuni zake zimeainisha baadhi ya misingi ya maadili inayopaswa kuzingatiwa ambayo ni Uadilifu, Uwazi, Uwajibikaji , Uaminifu na ukweli, matumizi sahihi ya taarifa , kuepuka mgongano wa maslahi, kutenda haki na kutopendelea, Kuheshimu Sheria pamoja na kutokupokea zawadi .

Bi. Jasmin aliendelea kuelezea kusema kuwa watumishi wa Umma pamoja na Viongozi wa Umma wanatakiwa kuwa na huruma, kuwa wasikivu , wanapotekeleza majukumu yao kujitolea kusaidia wengine kuwa natabia na mienendo mema inayokubalika katika jamii,kuwa mnyenyekevu, kujizuia na tama,kuwa tayari kukubali kukosolewa kufikiri kwa makini kbla ya kutenda pamoja na mengine mengi yenye maadili mema.

Bi Jasmin alieleza kuwa endapo watumishi na Viongozi wa Umma watazingatia misingi hiyo ya maadili itasaidia serikali kupata matokeo chanya katika kila idara na wananchi kuwa na imani na serikali yao kwani watumishi wanafanya kazi kwa niaba ya serikali.

Aidha Bi.Jasmin aliongeza kuwa watumishi wa Umma na Viongozi wa Umma wanapaswa kuzingatia maaadili kwa kiwango cha juu kwani maadili ni kinga ya maovu yote .’’Yatupasa kila wakati kupima faida na madhara ya matendo yetu na kuamua kutenda jambo sahihi wakati wote’’ alisema.

Pamoja na hayo Bi. Jasmin alibainisha kuwa watumishi wa umma pamoja na viongozi wa umma wanapokua waadilifu husaidia kupungua kwa makosa ya rushwa na makosa mengine. Hivyo basi kila kiongozi na mtumishi wa Umma anapaswa kuwa muadilifu katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku. ‘’Uadilifu unaanza ndani ya nafsi yako mwenyewe huwezi kutoa kitu ambacho huna’’alisema.

Ni wajibu wa kila Kiongozi na kila mtumishi wa Umma kukuza na kudumisha uadilifu na kulinda rasilimali za Umma nchi kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya Taifa.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >