JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Watumishi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Arusha Wakumbushwa kutopokea zawadi sizizoruhusiwa Kisheria.
27 Oct, 2023
Watumishi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Arusha Wakumbushwa kutopokea zawadi sizizoruhusiwa Kisheria.

Watumishi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Arusha Wakumbushwa kutopokea zawadi sizizoruhusiwa Kisheria.

Watumishi wa Umma wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Arusha wametakiwa kutopokea zawadi zisizoruhusiwa kisheria.

Hayo yameelezwa na Bw. Adam Kuhanda Afisa wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini katika mafunzo maalum ya maadili kwa Watumishi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Arusha.

Bw. Kuhanda alisema kuwa watumishi wa umma hawapaswi kupokea zawadi zisizoruhusiwa kisheria kwani kwa kufanya hivyo zinaweza kuwapelekea kujiingiza katika mgongano wa maslahi ambao unaweza kuathili utendaji wao wa kazi.

Katika mafunzo hayo mbayo msisitizo mkubwa uliwekwa katika maeneo nane (8) yanayohusu tabia na mienendo ya kimaadili ambayo watumishi wa umma wanapaswa kuyazingatia, Bw. Kuhanda aliyataja maeneo hayo kuwa ni pamoja na kutoa huduma bora; utii kwa serikali na kutoa huduma bila upendeleo.

Kwa mujibu wa Bw. Kuanda maeneo mengine ni kufanya kazi kwa uadilifu; kuwajibika kwa umma na kuheshimu Sheria na matumizi sahihi ya taarifa.

Akitoa ufafanuzi kuhusu kutoa huduma bora kwa wananchi, Bw. Kuhanda aliwaeleza watumishi hao kuwa mtumishi wa umma anapaswa pamoja na mambo mengine kuzifahamu vema na kuziheshimu kanuni za maadili, kuweka malengo halisi ya kazi ili kukuwezesha kufikia kiwango cha juu kabisa katika utendaji wako wa kazi; kuwa na ubunifu na siku zote kujibidiisha kuongeza viwango vya utendaji kwa kujiongezea maarifa na ujuzi.

Kuhusu kufanya kazi kwa uadilifu Bw. Kuhanda aliwaeleza watumishi kuzingatia mipaka ya madaraka yako na wasiyatumie kwa manufaa binafsi na kuwakandamiza wengine, kuepuka madaraka yao kupendelea marafiki au jamaa zao pamoja na kusimamia vizuri fedha na mali za umma walizokabidhiwa ikiwemo kuzuia uharibifu, ubadhirifu na upotevu.

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imejiwekea utaratibu wa kuwajengea uwezo wadau wake hususani Viongozi na watumishi wa umma pamoja na wananchi kuhusu Maadili kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma pamoja na Mafunzo hayo hufanyika kila mwaka ili kuwajengea uwezo watumishi wa mamlaka hiyo ili waweze kufanya kazi zao kwa uadilifu na kuzingatia sheria.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >