JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Watumishi wa Maadili “Wapigwa Msasa” kuhusu mbinu za kiuchunguzi.
27 Oct, 2023
Watumishi wa Maadili “Wapigwa Msasa” kuhusu mbinu za kiuchunguzi.

Watumishi wa Maadili “Wapigwa Msasa” kuhusu mbinu za kiuchunguzi.

Watumishi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wamepewa mafunzo juu ya mbinu mbalimbali za kiuchunguzi.

Mafunzo hayo ya siku nne yalifanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Kilimo cha Sokoine mjini Morogoro.

Akifungua mafunzo hayo Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji wa Rufani Sivangilwa Mwangesi alisema kuwa mafunzo hayo yanayolenga kuwajengea uwezo Maafisa Uchunguzi wa taasisi katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku na yataboresha utendaji kazi wa taasisi.

Aidha Mhe. Mwangesi alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia kuwajengea uwezo na kuwapa mbinu bora za kufanya chunguzi mbalimbali, ukusanyaji na uchambuzi wa vielelezo, namna bora ya kufanya mahojiano, uchunguzi kwa njia ya mtandao, uandishi wa taarifa ya uchunguzi na kuendesha kesi katika Baraza la Maadili.

“Mafunzo haya ni muhimu sana kwenu kwani yatawajengea uwezo na kuondoa ombwe ambalo limekuepo wakati wa kufanya mahojiano, uchunguzi, ukusanyaji wa vielelezo na uandishi wa taarifa za uchunguzi” alisema.

Katika hatua nyingine Kamishna wa Maadili aliongeza kuwa mafunzo hayo yatasaidia kuwajengea uwezo wa kufanya uchambuzi na uchunguzi wa nyaraka za fedha pamoja na uhalifu unaoweza kufanywa kwa ulaghai katika miamala, mikopo, hundi na mambo mengine yanayohusiana na fedha kwa viongozi wa umma ambapo ni uvunjifu wa kimaadili.

Mada mbalimbali zitawasilishwa na wakufunzi tofauti ikiwa ni pamoja na namna ya kutambua na kudhibiti mgongano wa maslahi, na Kanuni zake, mbinu za uchunguzi, ukusanyaji na uchambuzi vielelezo na uchunguzikwa njia ya mtandao.

Mafunzo hayo yamefadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB).

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >