JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Watumishi wa Maadili waaswa kuwa waadilifu.
27 Oct, 2023
Watumishi wa Maadili waaswa kuwa waadilifu.

Watumishi wa Maadili waaswa kuwa waadilifu.

Watumishi waOfisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wametakiwa kuyazingatia na kuyaishi yote yaliyopo katika kiapo cha Ahadi ya Uadillifu kwa Viongozi na Watumishi wa Umma .

Hayo yalisemwa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji wa Rufani Sivangilwa Mwangesimara baada ya kuongoza kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi wa Umma na Ahadi ya Uadilifu kwa Watumishi wa Umma kwa baadhi ya watumishi wa Sekretarieti ya Maadili. Tukio hilo lilifanyika tarehe 14 Septemba 2021 katika Ukumbi wa Ofisi hiyo Jijini Dodoma.

“Nawasii katika utekelezaji wenu wa majukumu kuyaishi mliyoapa katika Ahadi ya Uadilifu,” alisema.

Ahadi ya Uadilifu ni tamko rasmi na bayana la kimaandishi linalotolewa na Viongozi wa Umma, Watumishi wa Umma na Sekta binafsi kuonesha dhamira ya kuzingatia misingi ya maadili na Mapambano Dhidi ya Rushwa.

Mhe. Kamishna aliwaasa Watumishi hao kufanya kazi kwa Uadilifu, Uwajibikaji, weledi, uzalendo na kuepuka mgongano wa maslahi katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku kama walivyoahidi kwenye kiapo chao.

Jumla ya watumishikumi na sita waliohamia Sekretarieti ya Maadili hivi karibuni wameapa kiapo cha Ahadi ya Uadilifu Ikiwa ni Ishara ya Uadilifu na Uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu ya watumishi wa Umma.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >