JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

WATUMISHI WA KANDA YA KUSINI MTWARA WAMETAKIWA KUWA WAADILIFU:
29 Aug, 2023
WATUMISHI WA KANDA YA KUSINI MTWARA WAMETAKIWA KUWA WAADILIFU:

Watumishi wa Kanda ya Kusini Mtwara, wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa Uadilifu, Umakini, na weledi wa kiwango cha juu.

Kauli hiyo, imetolewana Kamishna wa Maadili Mhe, Jaji Sivangilwa Mwangesi, katika ziara yake ya kutembelea Kanda ya kusini Mtwara tarehe 21 juni, 2023.

Aidha, Mhe Mwangesi katika hotuba yake ameongeza kuwa, ziara hiyo ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma iliyoanza rasmi tarehe16 juni, na kuhitimishwa tareha 23 juni, 2023.

Mhe, Kamishna alifafanua kuwa,lengo kubwa la ziara yake katika maadhimisho haya ni pamoja na kuwakumbusha watumishi na viongozi wa Umma kwa ujumla kuhusu wajibu wao, na maadili katika kutekeleza majukumu yao ya kilasiku.

Kuhusu changamoto zilizopo katika kanda hiyo, Mhe, Mwangesi alifafanua kuwa, kuhusu uhaba wa watumishi na upungufu wa magari , suala hio linafanyiwa kazii na mchakato unaendelea.

Mhe, Mwangesia mewataka watumishi wa Kanda hiyo kutunza jengo la Ofisi ambalo ni zuri na kubwa ili lweze kudumu kwa muda mrefu ikiwani sehemu ya uboreshaji wa mazingira ya kufanyia kazi.

Aliongeza kuwa, Sekretarieti iko katika mchakato wakuanzisha mfumo wa Online Decrelation Systerm(ODS )ambao utasaidia kurahisisha utekelezaji wa Majukumu ya Taasisi na pia kuwawezesha Viongozi kutuma matamko yao kwa njia ya Mtandao kwa uhakika na urahisi zaidi tofauti na ilivyo sasa.

Ziara hii ya Mhe, Kamishna wa Maadili ,katika Kanda ya kusini Mtwara ni iMaadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kitaifa iliyoanza rasmi tarehe 16 juni, na kuhitimishwa tarehe 23 Juni, 2023.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >