JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

WATUMISHI SEKRETARIETI YA MAADILI WAPIGWA MSASA KUHUSU UCHUNGUZI WA KIDIGITALI.
27 Jan, 2025
WATUMISHI SEKRETARIETI YA MAADILI WAPIGWA MSASA KUHUSU UCHUNGUZI WA KIDIGITALI.

 

 

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambao ni wachunguzi pamoja na watunza kumbukumbu wamepatiwa mafunzo maalum ya mbinu mpya za kiuchunguzi na utunzaji wa siri.

Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika mkoani Iringa tarehe 27 Januari,2025 katika ukumbi wa Mount Royal Hoteli, Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Mst) Sivangilwa Mwangesi alieleza kuwa kutokana na ukuaji wa Teknolojia ni dhahiri kuwa wachunguzi wanapaswa kuongezewa uwezo wa namna bora ya kufanya uchunguzi wa kidijitaji ili kuboresha ufanisi katika uchunguzi hususan katika matumizi ya Teknolojia za kisasa ambazo husaidia kupata  taarifa nyingi kwa haraka na zenye usahihi.

“Katika mafunzo haya mtaweza pia kuongeza uelewa katika eneo la uchunguzi katika maeneo maalumu mathalan eneo linalozidi kukua la uchunguzi wa miamala ya kielektroniki hususan fedha za kidijitali” alisema.

Katika hatua nyingine Mhe. Mwangesi alieleza kuwa mafunzo hayo yatawasaidia watunza kumbukumbu kuelewa namna ya kuhifadhi taarifa za kiuchunguzi kwa usalama zaidi ili kupuka uvujaji wa taarifa hizo.

“Katika mafunzo haya, mtajifunza kuhusu utunzaji wa kumbukumbu kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu. Mtajifunza namna ya menejimenti ya kumbukumbu kwa mifumo iliyoanzishwa na Serikali kwa lengo la kuongeza tija na kuimarisha usalama na usiri wa taarifa nyeti” alisema.

Awali akitoa neno la utangulizi katika mafunzo hayo Katibu Idara ya Usimamizi Maadili kutoka Ofisi ya Rais Sekrtarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Kassim Mkwawa alieleza kuwa dhumuni kubwa la mafunzo hayo ni kuhakikisha kwamba watumishi hao wanakua na uelewa wa kutosha wa namna ya kufanya uchunguzi hususan katika miamala ya kielektroniki.

Bw. Mkwawa alieleza kuwa mafunzo hayo yataangazia mambo muhimu kama vile kutambua viashiria vya ukiukwaji wa maadili katika miamala ya kielektroniki, kutumia mbinu na zana za uchunguzi wa kidijitali, na kuelewa sheria zinazohusiana na ushahidi wa kielektroniki.

 

“Katika mafunzo haya tutajifunza mbinu kama vile kuhoji mashahidi kwa ufanisi, kufanya ukaguzi wa kina wa historia ya lalamiko, na kutumia zana za uchambuzi za kisasa zitakazosaidia kushughulikia malalamiko au masuala kuhusiana na miamala ya kielektroniki ambao kiuhalisia siyo rahisi kuchunguza iwapo hauna ujuzi na maarifa”,alisema.

Mafunzo hayo ya siku tano yatatolewa na wakufunzi kutoka Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma pamoja na wakufunzi kutoka Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa.

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >