JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

WATUMISHI SEKRETARIETI YA MAADILI WAASWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI
12 Mar, 2025
WATUMISHI SEKRETARIETI YA MAADILI WAASWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

 

WATUMISHI SEKRETARIETI YA MAADILI WAASWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

Watumishi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma  wamesisitiwa kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia maadili  bila kuyumba au kuyumbishwa  katika shughuli zao za kila siku.

Hayo yemesemwa na  Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi wakati akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Rais, Sekretareiti ya Maadili ya Viongozi uliofanyika Makao Makuu ya ofisi hiyo jijini Dodoma tarehe 12 Machi, 2025.

‘’Tusikubali kuyumba au kuyumbishwa na hatimaye kutolewa kwenye mstari, tuendelee kufuata misingi ya weledi na maadili katika utendaji kazi kwa kuepuka rushwa na kushinda vishawishi   na tamaa nyinginezo,’’alisema Mhe. Mwangesi.

Jaji Mwangesi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo ameongeza kuwa kwa kukubali kuwa mtumishi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, basi ni lazima uwajibike kwa  kuzingatia nidhamu, uaminifu, uwazi na kupendana.

"Kwa mara nyingine niwakumbushe  kuwa tunatakiwa kuwajibika kwa kuzingatia nidhamu, uaminifu, uwazi na kupendana na yeyote atakayeenda tofauti na hayo, atakuwa si miongoni mwetu na hatutasita kuchukua hatua stahiki dhiki yake," alisisitiza Jaji Mwangesi.

 Katika hatua nyingine Jaji Mwangesi amewakumbusha  baadhi ya watumishi wenye changamoto za kiuadilifu na kuwakumbusha  kuhakikisha kuwa wanakua mstari wa mbele katika   kuzingatia uadilifu na kufanya kazi kwa uzalendo.

‘’Ninafahamu kuna baadhi yetu wana changamoto za kiuadilifu katika utendaji wao, lakini kwakuwa Taasisi yetu tunayoitumikia ni ya kimaadili basi hatuna budi kukumbushana kwa lengo la     kujipa muda kujitathmini na kujirekebisha kwenye suala la uaminifu, nidhamu, kupendana pamoja na utii kwa mamlaka na viongozi waliopo juu yetu," aliongeza.

Aidha, Jaji Mwangesi amewataka wajumbe wa Baraza hilo kuwa mabalozi kwa watumishi wengine kwenye suala la ujazaji wa majukumu katika mfumo wa e-utendaji ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Serikali.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >