JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

WANANCHI WAKUMBUSHWA WAJIBU WAO WA KUKUZA NA KUSIMAMIA MAADILI.
20 Feb, 2024
WANANCHI WAKUMBUSHWA WAJIBU WAO WA KUKUZA NA KUSIMAMIA MAADILI.

Wito  huo umetolewa kwa wananchi nchini kupinga na kukataa kila aina ya uovu katika jamii ikiwemo rushwa, uonevu, wizi, ubadhirifu wa mali za umma na ya watu binafsi.

 

Katibu Msaidizi, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazini, Arusha Bw. Gerald Mwaitebele ametoa wito huo tarehe 20.2.2024 wakati akitoa mada ya Maadili ya Viongozi wa Umma kupitia kituo cha redio cha Arusha One FM kilichopo jijini Arusha.

 

Bw. Mwaitebele amesema, “Kila mwananchi anawajibika kukuza na kusimamia maadili nchini yakiwemo maadili ya Viongozi wa Umma.”

 

Kwa mujibu wa Katibu Msaidizi, ni wajibu wa wananchi kuisaidia Serikali kwa kutoa taarifa zitakazowezesha kuchukua hatua za kisheria na kinidhamu kwa watumishi wa umma wanaotumia vibaya madaraka kinyume na misingi ya Maadili.

Ameitaja baadhi ya misingi hiyo kuwa ni kutoa huduma  bila upendeleo, kutowaonea watu, kuepuka vitendo vya rushwa na kutumia mali ya umma kwa maslahi yao binafsi.

”Elimu hii tunayoitoa inalenga kuhimiza uadilifu katika maeneo ya kazi kwani utamaduni wa maadili unapojengeka katika jamii unasaidia kupunguza vitendo viovu katika jamii kwa kuwakumbusha viongozi wa umma kuzingatia maadili na kuwafichua viongozi wanaotumia madaraka yao vibaya,”alisema.

Katika hatua nyingine Bw. Mwaitebele aliwataka wananchi kuchagua viongozi waadilifu katika chaguzi zijazo na kuelimisha wenzao kuhusu masuala ya maadili na utawala bora.

 “Tunapoelekea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni vyema wananchi kuzingatia sifa za mtu muadilifu katika jamii ili kupata kiongozi muadilifu,” alisema.

Amezitaja baadhi ya sifa hizo kuwa ni usikivu, kutenda haki, kufanya kazi kwa bidii, kuwa mwaminifu katika hali zote na kufikiria kwa umakini kabla ya kutenda jambo lolote.

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >