JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Walezi wa Klabu za Maadili waswa kuwa na maadilii
27 Oct, 2023
Walezi wa Klabu za Maadili waswa kuwa na maadilii

Baadhi ya walezi wa klabu za maadili ambao ni waalimu kutoka shule za Sekondari na Msingi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamepatiwa mafunzo kuhusu maadili. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa shule ya Sekondari Dodoma tarehe 28 Oktoba, 2022.

Akifungua mafunzo hayo Kaimu Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya kati –Dodoma Bi. Modesta Mtui alisema kuwa walezi wa Klabu za maaadili wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuwa na maadili mema kwani mtoto anachokiona ndicho atakachokiishi hivyo mwalimu yeyote ni kioo kwa wanafunzi wake “Ni ngumu sana kwa mwalimu ambaye hana maadili kumfundisha mwanafunzi kuwa na maadili mema na mwanafunzi akaelewa’’’alisema.

Bi. Modesta alisema kuwa lengo la mafunzo hayo kwa walezi wa klabu hizo ni kupata uelewa wa pamoja juu ya dhana panaya maadili ili walezi hao wa klabu za maadili wawasaidie wanafunzi kuyaishi yale wanayofundishwa jambo litakalo wasaidia kuwa waadilifu toka utotoni hata watakapokua wakubwa.

Bi. Modesta alieleza kuwa Serikali kupitia Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambacho ndio chombo kikuu cha usimamizi wa maadili ya Viongozi nchini , iliona ni vyema kueneza maadili kwa wanafunzi walioko ngazi mbalimbali za masomo kama vile shule za msingi, sekondari pamoja na vyuo vikuu kwa kuanzisha klabu za maadili ikiaminika kuwa tabia na mienendo mwema kwa binadamu hufundishwa tangu akiwa mdogo na hasa akiwa shuleni au chuoni.

Aidha Bi. Modesta alisema kuwa Lengo la kuanzishwa kwa klabu za maadilini kuwajengea wanafunzina wanavyuo misingi bora ya maadili tangu wakiwa Shuleni na Vyuoni. Klabu hizo pia zitasaidia kuwatengeneza mabalozi wazuri wa Sekretarieti ya Maadili watakaosaidia kueneza na kuelimisha familia zao kwa ujumla juu ya suala la maadili. Klabu hizo pia zitawasaidia wanafunzi kujitambua na kujipambanua kitabia na kuachana na mienendo isiyofaa.

Akibainisha changamoto wanazokutana nazo walezi wa klabu za maadili ambao ni waalimu wa shule mbalimbali Mwalimu Marcus Magwa ambaye ni mlezi wa klabu ya maadili katika Shule ya Sekondari Dodoma alisema kuwa kutokana na kukua kwa utandawazi kwa sasa watoto wengi wanapata misukumo ya mienendo mibaya kutoka kwenye mitandao jambo linalowafanya watoto hao kuona kuwa kuwa na maadili ni ushamba mfano katika suala la mavazi mtoto anaona kuvaa nguo zinazomstiri mwili wake ni jambo lililopitwa na wakati.

Aidha Mwalimu Marcus alitoa wito kwa wazazi kutenga muda wa kukaa na watoto wao na kufuatilia mienendo yao ili kuweza kubaini mapema iwapo mtoto ana mienendo isiyofaa ili washirikiane na waalimu kuweza kudhibiti hali hiyo mapema .

Pamoja na hayo Mwalimu Marcus alitoa rai kwa Sekretarieti ya Maadili kuongeza kasi ya kueneza maadili nchini hususan kutoa elimu ya mara kwa mara kwa wanachama wa klabu ya maadili ili kuendana na kasi ya ukuaji wa utandawazi nchini ’’ utandawazi una nguvu unakua kwa kasi sana’’ alisema.

Katika mafunzo hayo walezi wa klabu za maadili watapata uelewa wa pamoja juu ya shughuli zinazotekelezwa na Sekretarieti ya Maadili, majukumu ya Sekretarieti ya Maadili .Katika mafunzo hayo walezi wa klabu za maadili watapata fursa yakupitia mwongozo wa kuanzisha na kuendesha klabu za maadili katika shule za msingi, Sekondari na Vyuo vya elimu Tanzania na kutoa maoni yao juu ya namna bora yautekelezaji wa mwongozo huo.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >