JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

WAKUU WA WILAYA WAPYA WATAKIWA KUHESHIMU NA KUVIISHI VIAPO VYAO
27 Oct, 2023
WAKUU WA WILAYA WAPYA WATAKIWA KUHESHIMU NA KUVIISHI VIAPO VYAO

Katibu Msaidizi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati Dodoma Bibi Jasmin Awadh i amewataka Wakuu wapya wa Wilaya walioteuliwa hivi karibuni kuheshimu na kuviishi viapo vyao walivyoviapa kwa uadilifu na uaminifu mkubwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Bibi Awadhi alitoa kauli hiyo alipokuwa akiongoza kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa Mkuu wa wilaya ya Chemba Mhe. Gerald Lomward Mongela katika hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Ofis i ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma tarehe 30 Januari 2023.

Alisema, “hakikisheni mnajitoa kutumikia viapo mlivyotoa mbele yetu na kuviweka katika kumbukumbu zenu za kila siku ili viwasaidie kuyakumbuka yale yote yaliyoelezwa katika viapo hivyo mnapotekeleza majukumu yenu ya kila siku.”

Katika hatua nyingine Bibi Awadhi alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Chemba kwa kuteuliwa kwake na alisema kuwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekupa heshima kubwa ya kuiongoza wilaya ya Chemba.

Katibu huyo Msaidizi pia aliwapongeza wakuu wengine wapya wawila ya za Bahi Mhe. Godwin Gondwe na Mpwapwa Mhe. Sophia Kizigo waliohamishiwa mkoani Dodoma katika mabadiliko ya vituo vya wakuu wa wilaya yaliyofanyika hivi karibuni.

Awali Mhe. Rosemary Senyemule Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alimwapisha Mhe. Gerald Lomward Mongela kuwa Mkuu wa wilaya ya Chemba, hafla hiyo pia iliudhuriwa na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Dodoma wakiwemo Viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa pamoja na Manejimenti ya ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Dodoma.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >