JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

PO-ETHICS SECRETARIAT Logo
Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu wajengewa uwezo juu ya Sheria ya Maadili ya Maadili ya viongozi wa Umma.
29 Apr, 2026
Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu wajengewa uwezo juu ya Sheria ya Maadili ya Maadili ya viongozi wa Umma.

Wakurugenzi wa Utawala na  Rasilimaliwatu kutoka  kaika Wizara na Taasisi mbalimbali  za  umma  wamejengewa uwezo juu ya Sheria ya Maadili ya Maadili ya viongozi wa umma  sura ya 398 [marejeo ya 2023]. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Zabibu Hotel Mkoani Dodoma tarehe 29 Aprili, 2026.

Akifungua mafunzo hayo Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Stahiki) Sivangilwa Mwangesi alisema kuwa Ofisi yake imeandaa mafunzo mahsusi kwa Wakurugenzi wa Utawala na  Rasilimali watu kwa lengo la kuwajengea uelewa wa kina kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma pamoja na kuwapa ujuzi wa namna ya kutumia Mfumo wa Kielektroniki wa Uwasilishaji wa Matamko ya Mali na Madeni  kwa njia ya mtandao.(Online Declaration System – ODS).

“Mafunzo haya yameandaliwa mahsusi kwa ajili yenu, kwa kutambua nafasi yenu ya kipekee katika kusimamia rasilimali watu ndani ya Taasisi za Umma, pamoja na jukumu lenu muhimu katika kuhakikisha utekelezaji wa misingi ya maadili katika utumishi wa umma” alisema.

Katika hatua nyingine  Mhe. Jaji alisisitiza suala la Maadili kwa Viongozi wa Umma na kusema kuwa  Maadili yanaanza na Kiongozi mwenyewe “Maadili siyo jambo la ziada  katika utumishi wa umma, Bila maadili, hakuna uaminifu; na bila uaminifu, hakuna Utawala Bora” alisema.

Aidha Mhe.  Mwangesi katika hotuba yake aliwakumbusha viongozi hao juu ya wajibu wao wa kisheria wa kutoa matamko  ya Raslimali na madeni ndani ya muda uliowekwa ambapo  kwa sasa Viongozi hao wanatoa matamko  hayo kwa njia ya mtandao.

“Kama mnavyofahamu, mfumo huu wa kujaza matamko kwa njia ya mtandao   ODS umeanzishwa ili kuboresha uwazi, ufanisi na urahisi katika utekelezaji wa matakwa ya kisheria ya utoaji wa matamko. Kupitia mfumo huu, viongozi wa umma wanaweza kuwasilisha taarifa zao kwa njia ya kisasa, salama na inayorahisisha ufuatiliaji na uhakiki”alisema.

Mhe Mwangesi pia  aliwasisitiza viongozi  hao  kutoa taarifa kwa wakati kwa Sekretarieti ya Maadili kuhusu watumishi wote wanaoteuliwa au kupandishwa vyeo na kuingia katika nafasi za uongozi wa umma ili kuwezesha usajili wa viongozi hao katika mifumo ya Sekretarieti, hususan mfumo wa ODS na kuwaelekeza viongozi hao juu ya wajibu wao wa kisheria wa kutoa matamko ndani ya muda uliowekwa, na kusimamia ufuatiliaji wa utekelezaji wa wajibu huo ndani ya taasisi zao.

Mada mbili ziliwasilishwa katika mafunzo hayo ikiwa ni mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma pamoja na mada kuhusu namna ya ujazaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni kwa njia ya mtandao (ODS)

 

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >