JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Wajumbe wa Kamati ya Ukaguzi wapatiwa mafunzo kuhusu ukaguzi.
27 Oct, 2023
Wajumbe wa Kamati ya Ukaguzi wapatiwa mafunzo kuhusu ukaguzi.

Wajumbe wa Kamati ya Ukaguzi na Menejimenti ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wamepatiwa mafunzo kuhusu ukaguzi. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma tarehe 20 Septemba,2022.

Akifungua mafunzo hayo Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi alisema kuwa katika kuhakikisha Kamati ya Ukaguzi inaendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, Sekretarieti ya Maadili imeandaa mafunzo hayo muhimu yatakayoshirikisha wajumbe wa kamati pamoja na menejimenti ili kuwa na uelewa wa pamoja katika namna bora ya uendeshaji na usimamizi wa Taasisi.

Mhe. Mwangesi alieleza kuwa Kamati ya Ukaguzi ina kazi muhimu sana ya kutoa ushauri kwa Afisa Masuuli kuhusu masuala ya uendeshaji wa Taasisi katika maeneo ya menejimenti ya vihatarishi, mifumo ya udhibiti na masuala ya utawala bora kwa ujumla.

Pamoja na hayo kamati ya ukaguzi inatoa ushauri katika masuala mbalimbali ya uendeshaji wa Taasisi hususani usimamizi wa fedha, rasilimali watu, shughuli mama za Taasisi, manunuzi na masuala mengine mengi jambo ambalo limeisaidia Taasisi kupata hati inayoridhisha ya ukaguzi.

Aidha Mhe. Mwangesi aliendelea kusema kuwa Kamati ya Ukaguzi kupitia ushauri wake inasaidia sana kuleta imani kwa wadau juu ya Taasisi inavyoendeshwa.

Mafunzo hayo ya siku mbili yatawapa washiriki fursa ya kufahamu namna shughuli kuu za Taasisi (Bussiness Process) zinavyofanyika na kuwawezesha washiriki kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >