JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR WATEMBELEA MAKAO MAKUU SEKRETARIETI YA MADILI YA VIONGOZI WA UMMA.
29 Aug, 2023
WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR WATEMBELEA MAKAO MAKUU SEKRETARIETI YA MADILI YA VIONGOZI WA UMMA.

Wajumbe wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi, Zanzibar inayoshughulikia viongozi wakuu tarehe 22 Agosti, 2023 imetembelea ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma jijini Dodoma kwa lengo la kujifunza jinsi taasisi hiyo inavyotekeleza majukumu yake.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Mchano Othman Said amesema,“tumekuja hapa Dodoma kwa lengo la kujifunza jinsi taasisi yenu inavyofanya kazi.”

Wajumbe wengine wa Kamati hiyo walioshiriki katika ziara ni; Mhe. Mussa Foum Mussa, Mhe. Abdalla Abbas Wadi, Mhe. Maryam Thani Juma, Mhe. Zena Abdallah Salum, Mhe. Haji Shaaban Waziri, Mhe. Ali Alawy Ali, Mhe. Mwaisha Mohammed Kheir, Mhe. Shawana Mohammed Haji, Mhe.Amina Abeid Hemed na Mhe. Massoud Ali Hamad.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ameomba Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kufanyakazi kwa kushirikiana na Tume ya Maadili ya Zanzibar.

“Naomba ofisi hii ifanyekazi kwa kushirikiana na Tume ya Maadili Zanzibar ili kukuza Maadili ya Viongozi wa Umma nchini,” amesema.

Kwa upande wake Mhe. Sivangilwa mwangesi, Kamishna wa Maadili amewaeleza wajumbe wa kamati kuwa changamoto kubwa inayoikabili Sekretarieti ya Maadili ni, uelewa mdogo wa wananchi kuhusu maadili ya Viongozi wa Umma.

“Wananchi wengi hawana uelewa kuhusu ukiukwaji wa Maadili ya Viongozi wa Umma jambo linalosababisha kutotoa taarifa katika taasisi yetu kuhusu viongozi wanaokiuka maadili kwa mujibu wa Sheria,” amesema.

Amezitaja changamoto nyingine kuwa ni baadhi ya viongozi wa umma kuwa mbali kijiografia kutoka mahali zilipo ofisi zetu na uelewa mdogo wa matumizi ya Teknoloji ya Habari na Mawasiliano kwa wananchi.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >