JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

WAHESHIMIWA MAHAKIMU MKOA WA KILIMANJARO WAASWA KUJIEPUSHA NA MGONGANO WA MASLAHI
27 Oct, 2023
WAHESHIMIWA MAHAKIMU MKOA WA KILIMANJARO WAASWA KUJIEPUSHA NA MGONGANO WA MASLAHI

Mahakimu wa mkoa wa Kilimanjaro wametakiwa kujiepusha na vitendo mbali mbali vinavyopelekea kuwepo kwa mgongano wa Maslahi.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Msaidizi kanda ya kaskazini Arusha Bi. Anna Mbasha alipokuwa akitoa mafunzo kwa mahakimu wa ngazi mbalimbali wa mkoa wa Kilimanjaro kuhusu maadili hivi karibuni.

Aidha, Bi. Mbasha alifafanua kuwa mgongano wa maslahi ni miongoni mwa matataizo ya kimaadili yanayozikumba nchi nyingi duniani na kwamba tatizo hili lina madhara makubwa kwa maendeleo ya nchi kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni lisipodhibitiwa.

“Mgongano wa Maslahi ni hali ya kukinzana kati ya maslahi binafsi ya kiongozi wa umma na kazi au majukumu yake kwa umma,” alisema.

Kwa mujibu wa Katibu huyo Msaidizi, maslahi binafsi yanaweza kuathiri utekelezaji wa majukumu ya Kiongozi kwa misingi ya haki na usawa, au upatikanaji wa ukweli.

Bi. Mbasha aliyataja mazingira yanayosababisha Mgongano wa Maslahi kuwa ni pamoja na Kudai, kuomba na kupokea zawadi, fadhila na maslahi ya kiuchumi yasiyostahili, kushindwa kutamka manufaa binafsi yanayoonekana moja kwa moja au vinginevyo katika Mkataba na Serikali pamoja na Matumizi ya rasilimali za umma kwa maslahi binafsi.

Mazingira mengine ni pamoja na matumizi mabaya ya magari ya umma, simu, kompyuta, kusaidia kampuni binafsi katika kupata kandarasi serikalini, kutumia muda wa saa za kazi kutekeleza shughuli za Kampuni binafsi na kushindwa kutamka maslahi binafsi katika mikataba na Serikali.

“Kiongozi wa Umma kutumia taarifa za utumishi wake uliopita kujinufaisha mwenyewe au kumsaidia mtu mwingine kupata manufaa binafsi, kupokea au kuomba fadhila au manufaakama vile usafiri, kulipiwa ada za shule, vitendo vyote hivi vinapelekea kuwepo kwa mgongano wa maslahi na pia ni ukiukaji wa Maadili kwa kiongozi wa Umma,” alisema.

Mafunzo haya ya Waheshimiwa Mahakimu yaliwashirikisha zaidi ya Mahakimu 60 wa ngazi mbali mbali wa mkoa wa Kilimanjaro

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >