JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Viongozi watakiwa kuepuka vitendo visivyo vya Maadili:
27 Oct, 2023
Viongozi watakiwa kuepuka vitendo visivyo vya Maadili:

Viongozi wa Umma wametakiwa kuepuka vitendo visivyo na maadili katika utekelezaji wa majukumu yao katika kuwatumikia wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu tawala wa mkoa wa Tabora Bw Daniel Barago alipokuwa akifungua mafunzo kuhusu sheria ya maadili ya viongozi wa umma kwa Viongozi wa mkoa huo yaliyofanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tabora tarehe 14 Februari 2023.

Bwana Barago katika hotuba yake amevitaja vitendo hivyo visivyo na maadili ambavyo ni utoajin wa huduma usioridhisha kwa wananchi, kujihusisha na mgongano wa maslahi, matumizi mabaya ya madaraka, wizi na ubadhirifu wa mali za umma, rushwa, unyanyasaji wa kijinsia, matumizi ya lugha chafu, na kwamba vitendo hivyo vinaashiria ukosefu wa maadili.

Aidha Bwana Barago alifafanua kuwa, ni muhimu kwa viongozi kutenda kazi kwa kuzingatia Maadili, kwani matumaini ya wananchi kwa serikali yao ni kuapatia huduma bora kwa wakati na bila upendeleo.

“Tanzania inahitaji kuwa na viongozi ambao ni mfano mzuri wa uzingatiaji wa maadili, unaozingatia Sheria, Kanuni na Taratibu katika utendaji wao wa kazi alisisitiza”

Katibu Tawala huyo katika hotuba yake alisisitiza kuwa kiongozi anatakiwa kutotumia vibaya raslimali za umma, kujizuia na mgongano wa maslahi, kutojilimbikizia mali na kutotumia madaraka yake vibaya na kwamba maadili hayo yamelenga katika kuhakikisha kuwa viongozi wa Umma wamatekeleza majukumu yao kwa uadilifu, uaminifu, uwazi, haki, kutopendelea na uwajibikaji ili kujenga, kudumisha na kulinda imani ya wananchi kwa viongozi na Serikali yao.

Bwana Barago aliongeza kuwa, Tanzania inahitaji kuwa na viongozi ambao ni mfano mzuri wa uzingatiaji wa maadili, wanaozingatia Sheria, Kanuni na Taratibu katika utendaji wao wa kazi na kwamba wana dhima ya kuhakikisha kuwa wanazingatia viwango vya juu vya maadili na kujiepusha na mgongano wa maslahi ili kuimarisha imani ya wananchi kuhusu uadilifu wao na katika utaratibu wa kufanya maamuzi ya Serikali.

Aliongeza kuwa, Kiongozi wa siasa au mtumishi yoyote wa umma anatakiwa atumie wadhifa wake kwa maslahi ya umma na wananchi kwa ujumla na sio kwa manufaa yake binafsi.

Mafunzo hayo kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma yamewashirikisha

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >