JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

VIONGOZI WAASWA KUZINGATIA MAADILI
06 Mar, 2025
VIONGOZI WAASWA KUZINGATIA MAADILI

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Reuben Shigella amewataka Viongozi wa Umma Mkoani humo kuzingatia maadili katika Utekelezaji wa majukumu yao hasa katika ujazaji wa Matamko yao kwa uadilifu,  uwazi na ukweli hasa katika kipindi hiki ambacho viongozi tunajaza matamko yetu kwa njia ya Mtandao.

Mhe, Shigella ametoa kauli hiyo alipokuwa akifungua mafunzo ya Maadili kwa viongozi wa Mkoa wa Geita yaliyoandaliwa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Ziwa, yaliyofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Ofisi ya  Mkuu wa Mkoa wa Geita Machi 6, 2025.

Katika hotuba yake Mhe, Shigella amefafanua kuwa kuanzishwa kwa mfumo huu mpya wa ujazaji wa matamko kwa nja ya  mtandao umesaidia sana katika kuwarahisishia viongozi kujaza matamko yao kwa haraka kwa usahihi na kwa muda unaotakiwa tofauti  na ilipokuwa hapo  awali ambapo ujazaji ulikuwa wa kujaza kwenye nakala ngumu.

Ameongeza kuwa uwepo huu wa teknolojia katika ujazaji wa matamko umesaidia pia  kuwawezesha viongozi kujaza matamko yao popote pale walipo bila kutumia muda mrefu kusafiri kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine kwa ajili ya kupeleka matamko yao.

Awali akiwakaribisha viongozi Katibu msaidizi Kanda ya Ziwa Bw. Godson Kweka amewataka viongozi wa umma mkoani Geita kutekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi kwa kutanguliza maslahi ya umma mbele na kukemea vitendo vinavyoashiria ukiukwaji wa maadili ya viongozi.

Mafunzo hayo yamewashirikisha viongozi wa umma wa mkoa wa Geita wakiwemo, wakurugenzi wa Halmashauri, wakuu wa Taasisi, wakuu wa Idara na Vitengo, wakuu wa wilaya pamoja na Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa.

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >