JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Viongozi waaswa kujali maslahi ya Umma
27 Oct, 2023
Viongozi waaswa kujali maslahi ya Umma

Viongozi waaswa kujali maslahi ya Umma

Viongozi wote wa Umma nchini wameaswa kujali maslahi ya Umma ambayo ndiyo msingi mkuu wa Serikali yeyote duniani.

Hayo yalisemwa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi alipokua akitoa mada katika kikao cha Viongozi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Tabora kilichofanyika tarehe 06 Agosti 2021 mkoani Tabora.

Mhe. Mwangesi alisema kuwa kiongozi yeyote wa Umma ni kioo cha jamii husika hivyo basi hana budi kujali maslahi ya Umma ikiwa ni pamoja na kuwa mzalendo kwa nchi yake, kufanya kazi kwa uaminifu,huruma,umakini,kijizuia na tamaa na kuzingatia viwango vya juu vya maadili pamoja na kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria taratibu na miongozo mbalimbali.

Mhe.Mwangesi aliongeza kuwa Viongozi wote wanapaswa kuwa na mienendo mizuri isiyotia shaka ili waweze kuaminikakatika jamiiinayowazunguka. Ni dhahiri kuwa kiongozi yeyote anapokua muadilifu kwa watu anaowaongoza bila shaka atapata heshima anayostahili katika jamii nan chi kwa ujumla

Mhe. Mwangesi alisisitiza kuwa “kiongozi ambaye ni muadilifu hufanya mambo mazuri hata pale ambapo hajaambiwa afanye ama pale ambapo hakuna anayemuona lakini kwa yule ambaye si muadilifu anaweza kufanya mambo mengi kwa kutumia nguvu na asifanikiwe hivyo nawaasa viongozi kuwa waadilifu jambo ambalo litarahisishautendaji utendekaji wa yale mambo ambayo wanataka yafanyike”.

Katika hatua nyingine Mhe. Mwangesi aliwakumbusha viongozi baadhi ya misingi ya maadili ikiwa ni pamoja nakufanya maamuzi kwa kufuata sharia,kanuni,miongozo kwa manufaa ya umma,kujiepusha na migongano ya maslahi,kutokua na mienendo ambayo itaaibisha utumishi wa Umma, kuzingatia sheria na mipaka ya matumizi ya madaraka na nyinginezo.

Awali akifungua kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt Batilda Buriani alisema kuwa Viongozi wote wanapaswa kuwa waadilifu na kuepuka mgongano wa maslahi

Mhe. Batilda alisema kuwa amefurahishwa na ziara ya Mhe Kamishna mkoani hapo kwani ni wazi kuwa ujio wake unawakumbusha viongozi kukumbuka na kujitathmini kupitia kiapo cha Ahadi ya Uadilifu walichoapa mara tuu walipoapishwa kuwa Viongozi.

Kikao hicho cha Kamishna wa Maadili na Viongozi wa Umma ni sehemu ya Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2021 ambapo Mhe. Mwangesi anatembelea wadau wa maadili, kutoa elimu na kusikiliza kero na malalamiko yao kwa lengo la kuboresha huduma zinazotolewa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >