JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Viongozi Wa Wa Umma Wametakiwa Kufanya Kazi Kwa Uadilifu
27 Oct, 2023
Viongozi Wa Wa Umma Wametakiwa Kufanya Kazi Kwa Uadilifu

Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi amewataka Viongozi wa umma kufanya kazi kwa uadilifu na uaminifu na kutojiingiza katika vitendo vinavyopelekea ukiukwaji wa maadili hasa mgongano wa maslahi katika utekelezaji wa Majukumu yao ya kila siku.

Mhe. Mwangesi ameyasema hayo katika kikao chake na Viongozi wa Mkoa wa Mwanza kilichokuwa sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma iliyoanza Juni 16 hadi Juni 23, 2022. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Kamishna Mwangesi alisema, “jiepusheni na shughuli zinazosababisha mgongano wa maslahi kwasababu mgongano wa maslahi umekuwa chanzo kikubwa cha uvunjifu wa maadili miongoni mwa Viongozi wa Umma.”

Kwa mujibu wa Mhe. Mwangesi, kiongozi wa umma kijihusisha na mgongano wa maslahi ni ukiukwaji wa misingi ya maadili kwani husababisha manung’uniko, kuathiri utendaji na tija kinyume na matarajio jambo ambalo huathiri taswira nzuri ya Serikali mbele ya wananchi.

“Endapo viongozi mtawajibika katika maeneo yanu ya kazi kwa uadilifu itajenga imani kwa wananchi mnaowaongoza na Serikali kwa ujumla,” alisema.

Kamishna Mwangesi aliwataka Viongozi wa mkoa wa Mwanza na Tanzania kwa ujumla kutojiingiza katika Mgongano wa Maslahi wanapotekeleza majukumu yao kwasababu kitendo hicho ni kinyume cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na 13 ya mwaka 1995 kwa mujibu wa ibara ya 132 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

“Ibara hii imekasimu majukumu ya Mhe. Rais yanayotajwa katika kifungu cha 5 (1) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, kusimamia na kukuza uadilifu wa viongozi wa umma,” alisema.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert GabrieL alisema kuwa Maadili ni hatua muhimu inayomtambulisha mtu ndani ya jamii husika na hujitokeza katika matendo yake.

“Maadili tunayozungumza hapa ni maboresho ya maadili yaliyo kwenye vitabu vyetu vya dini na bahati nzuri hapa hakuna mpagani,” alisema na kuongeza kuwa wapo baadhi ya viongozi wanakiuka maadili kwa kula zaidi ya kiasi wanachostahili kula.

“Tule kiasi chetu tulichopangiwa kwa kuwa ukila zaidi ya kiasi chako kitakuletea matatizo na utaishia mikononi mwa vyombo vya dola na kupata fedheha.”

Kwa mujibu wa Mhandisi Gabriel, lengo la kikao hiki ni kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika kupinga vitendo vya rusha, ufisadi, na matumizi mabaya ya fedha za Umma.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >