JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MGONGANO WA MASLAHI
23 Jan, 2024
VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MGONGANO WA MASLAHI

Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera Dkt. Abel Nyamahanga amewataka Viongozi wa Umma kuviishi viapo walivyo apa kikiwemo kiapo cha Ahadi ya Uadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao na kuepukana na vitendo vya mgongano wa maslahi ili kujenga imani ya wananchi wanaowaongoza.

Dkt. Nyamahanga ametoa kauli hiyo alipokuwa akifungua mafunzo ya Viongozi wa Umma kuhusu Maadili yaliyoendeshwa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba tarehe 23 Januari, 2024.

 “Serikali inatumia fedha nyingi kwenye miradi ya maendeleo kupitia katika halmashauri mbalimbali nchini hivyo, rasilimali hizo zinahitaji usimamizi mzuri wa Viongozi” amesema.

Dkt. Nyamahanga ameongeza kuwa Viongozi wa Umma wanayo dhamana kubwa katika kusimamia rasilimali za umma kwa umakini na uadilifu mkubwa ili kujenga imani kwa wananchi wanaowaongoza.

Amewataka viongozi kuzingatia maelekezo ya Serikali katika utendaji wa kazi kwa kufanya maamuzi sahihi kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo.

Awali akieleza lengo la mafunzo hayo Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Godson Kweka aliwakumbusha Viongozi kujiepusha na vitendo vyote vinavyopelekea uwepo wa mgogoro wa maslahi na kuwataka Viongozi hao kufanya kazi kwa uadilifu na uaminifu mkubwa ili kujenga imani kwa wananchi wanaowaongoza.

Bw. Kweka pia amewataka viongozi kusimamia rasilimali za umma kwa uadilifu mkubwa hasa pesa za miradi mbalimbali ya maendeleo katika halmashauri.

Kuhusu urejeshaji wa Tamko la Rasilimali na Madeni ya Viongozi wa Umma kwa mwaka jana 2023 amesema asilimia 90 ya Viongozi wote wa Halmashauri ya Muleba walirejesh Matamko yao kwa wakati.

Aidha mafunzo hayo ya Maadili ya Viongozi wa Umma yamehudhuriwa na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba zaidi ya 100 kutoka katika Idara, Vitengo pamoja na waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >