JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

VIONGOZI WA UMMA WAKUMBUSHWA KUREJESHA MATAMKO YAO KWA WAKATI:
21 Dec, 2023
VIONGOZI  WA UMMA WAKUMBUSHWA KUREJESHA MATAMKO YAO KWA WAKATI:

Jumla ya Viongozi wa Umma 2,475 kati ya 15,762 ndio wamerejesha Matamko yao ya Raslimali na Madeni hadi kufikia tarehe 20 Desemba 2023.

Taarifa iliyotolewa na Bw. Waziri Kipacha, Katibu Idara ya Usimamizi Maadili Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma tarehe 21.12.2023 jijini Dodoma, imeeleza kuwa idadi hiyo ni sawa na asilimia 16 ya viongozi wote wanaopaswa kurejesha Tamko la Raslimali na Madeni kwa  mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya mwaka 1995.

Bwana Kipacha katika taarifa yake kwa waandishi wa habari amewataja baadhi ya Viongozi ambao tayari wamekwisharejesha matamko yao  kwa  kamishna wa Maadili kuwa ni Mhesimiwa  Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Phillip Mpango, Makamu wa Rais, na Mhe, Kassim Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Bwana Kipacha amewataka viongozi wengine wa Umma ambao  bado hawajawasilisha matamko yao wakiwemo waliotamkwa katika Tangazo la Serikali Na. 857 la tarehe 24 Novemba, 2023 kuwa, “tangu siku ya tangazo hilo wanawajibika kutimiza masharti yote ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ikiwemo kuwasilisha Matamko yao kwa  Kamishna wa Maadili.”

Katika taarifa hiyo, Katibu huyo amesema kuwa, “kutokana na Mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imeanza kupokea Matamko hayo kwa njia ya Mtandao yaani ‘Online Declaration System- ODS’ ambapo Kiongozi anaweza kuingia katika mfumo kwa anuani ya https://ods.maadili.go.tz au kupitia tovuti ya www.maadili.go.tz na kubofya neno ODS hapo ataingia moja kwa moja na kujaza Tamko lake kwa urahisi zaidi.”

Kwa mujibu wa Bw. Kipacha, mfumo huu utawawezesha viongozi kujaza matamko yao kwa urahisi na kwa usahihi zaidi popote pale watakapokuwa iwe ndani au nje ya nchi na pia utamsaidia kiongozi kutosafiri umbali mrefu na kumpunguzia gharama za kupakua fomu za Tamko kuzijaza na kuzituma kwa njia ya posta ambapo hutumia gharama kubwa na muda mrefu kufika katika ofisi zetu kwa wakati. 

Ameitaja faida nyingine ya mfumo wa ODS kuwa ni kuepusha upotevu wa fomu katika zoezi la urejeshaji unaotokana na usafirishaji kwa njia ya posta na vyombo vingine vya usafiri pia mfumo huu utaondoa uwezekano wa kupokea matamko ya watumishi ambao sio Viongozi  kwa   Mujibu wa Shera ya Maadili ya Viongozi wa Umma na kwamba Kiongozi atakayejaza Tamko atakuwa ametengenezewa akaunti na Sekretarieti ya Maadili.

“Matamko yatakayopokelewa yatakuwa ya Viongozi wanaowajibika na Sheria ya Maadili  na Si vinginevyo.” amesema.

Bwana Kipacha amefafanua kuwa, kwa kuzingatia Sheria ya Maadili ya Viongoziwa Umma kifungu cha 9(1)(b) kinamtaka Kiongozi wa Umma kila mwisho wa mwaka kabla ya tarehe 31 Desemba kuwasilisha Tamko lake kwa Kamishna wa Maadili linaloonyesha Raslimali zake, au mume au watoto wake wenye umri usiozidi miaka 18 ambao hawajaoa au kuolewa.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >