JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Viongozi wa Umma mia sita hamsini na nane kuhakikiwa
27 Oct, 2023
Viongozi wa Umma mia sita hamsini na nane kuhakikiwa

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, inatarajia kuanza zoezi la uhakiki wa Raslimali na madeni ya viongozi wa umma kuanzia tarehe 7 Novemba hadi tarehe 18 Novemba 2022.

Jumla ya Viongozi wa Umma mia sita hamsini na nae (658) wanatarajiwa kufanyiwa uhakiki wa rasilimali namadeni yao ambapo zoezi hilo litafanyika katika mikoa ya Dar es salaam ,Njombe, Kilimanjaro, Lindi, Dodoma, Geita, Mwanza, Tabora, Tanga .

Kauli hiyo imetolewa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi alipokua akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini mapema wiki hii katika ukumbi wa Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jijini Dodoma.

Mhe. Kamishna katika taarifa yake alisema kuwa, pamoja na majukumu mengine yanayotekelezwa na Sekretarieti ya Maadili , Sekretarietiya Maadili inalo jukumu kubwa la kufanya uhakiki wa matamko ya rasilimali na madeni ya Viongozi wa Umma. “Zoezi hili hufanyika kwa awamu na katika awamu hii tumechagua idadi hiyo ya viongozi kufanyiwa uhakiki wa rasilimali na madeni yao” alisema.

Aidha Mhe. Kamishna alitoa rai kwa Viongozi wote waliochaguliwa kufanyiwa uhakiki huo kutoa ushirikiano wa hali na mali kwa timu zilizoteuliwa kufanya uhakiki katika maeneo yao pamoja na kufanya maandalizi kwa mujibu wa maelekezo yaliyotolewa kupitia barua walizotumiwa ili kuweza kurahisisha zoezi hili.

Aidha, Mhe. Kamishna alihitimisha taarifa yake kwa kuwakumbusha Viongozi wa Umma kutoa matamko ya Rasilimali,Maslahi na Madeni ya mwaka 2022 kwa mujibu wa kifungu cha 9 cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma,na kwamba mwisho wa kurejesha fomu hizo ni tarehe 31 Disemba, 2022. Aidha fomu hizo zinapatikana katika tovuti ya taasisi ambayo ni www.ethicssecretariat.go.tz.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >