JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

VIONGOZI ONGEZENI UWAZI, UWAJIBIKAJI KWA WANANCHI KUCHOCHEA MAENDLEO.
17 May, 2024
VIONGOZI ONGEZENI UWAZI, UWAJIBIKAJI KWA WANANCHI KUCHOCHEA MAENDLEO.

Viongozi wa Umma nchini wametakiwa kuongeza kasi ya utendaji kazi, kuchochea maendeleo kwa wananchi na kuzingatia maadili, uwazi na uwajibikaji wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku.

Wito huo umetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bi. Doris Ntuli Kalasa wakati akifungua mafunzo ya maadili kwa viongozi wa Taasisi mbalimbali za mkoa wa Iringa yaliyofanyika katika ukumbi wa VETA tarehe 17 Mei 2024.

Bi. Doris alisema kuwa maadili ndio kinga ya maozo yote katika jamii na ndio chimbuko la mafanikio katika maeneo mbalimbali kama vile elimu, maji, kijamii, kiutamaduni pamoja na kukuza utawala bora.

Kiongozi wa umma anatakiwa kubadilika kimtazamo na kifikra na kuzingatia kwa vitendo swala la maadili kwa kuwa kiongozi wa umma ni kioo cha jamii popote pale anapokuwepo,alisema, Bi. Doris Kalasa na kuongeza kuwa, “ndio maana kila wakati tunamsikia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akisisitiza Maadili kwa Viongozi wa Umma.

Aidha, Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, amewaagiza viongozi wa umma waliopata mafunzo kuandaa utaratibu wa kuyafikisha mafunzo kwa watumishi wote walio chini yao na maeneo wanayosimamia ili kulahisisha majukumu yao ya kila siku na kupunguza matukio ya uvunjifu wa maadili kwenye ofisi za umma.

“Naishukuru Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kuandaa mafunzo ambayo yatawasaidia Viongozi wa Iringa kujijenga kimaadili na kuwakumbusha wakati wote misingi ya maadili wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao,” Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa alisema.

Kwa upande wake Bw. Salvatory Kilasara, Katibu Msaidizi, Idara ya Ukuzaji Maadili, Sekretarieti ya maadili amewatoa hofu viongozi wa umma kuhusu ujazaji Tamko la Rasilimali na Madeni kuwa halina maana ya kuzuia kiongozi wa umma kumiliki mali.

Amesema, “kiongozi wa Umma haki ya kumiliki mali ila iwe ni mali halali.

Bw. Kilasara  amesema msingi wa mafanikio kwa kiongozi wa umma ni nidhamu na maadili ili kuondoa migongano na migogoro ya kazini na kuhakikisha kiongozi wa umma unaishi maisha yako na kurizika na unachopata na epuka kuishi Maisha ya watu wengine.

 

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >