JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Viongozi na Watumishi watakiwa kuwajibika:
29 Aug, 2023
Viongozi na Watumishi watakiwa kuwajibika:

Viongozi na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Chalinze wametakiwa kufanya kazi kwa kuwajibika kwa pamoja na kujiepusha na mgongano wa Maslahi, katika utendaji wao wa kila siku.

Kauli hiyo, imetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Archanus Kilaja alipokuwa akifungua mafunzo ya Maadili kwa viongozi na watumishi wa halmashauri hiyo yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo tarehe 23 Mei, 2023.

Aidha, Bwana Kilaja katika hotuba yake aliwaasa viongozi na watumishi hao, kuyaishi na kuyafanyia kazi yale yote waliojifunza katika kuboresha utendaji kazi wao wa kila siku kwa uadilifu na uaminifu mkubwa.

Bwana Kilaja ameiomba Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutoa mafunzo ya maadili kwa watumishi wengine wa Halmashauri hiyo ikiwemo idara ya Afya, Watendaji wa Kata na Vijiji na kwamba hao ndiyo wanaolalamikiwa zaidi na wananchi kukiuka maadili.

Naye Katibu Msaidizi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam Bi. Elizaberth Komba amewataka Viongozi na watumishi hao waliopata mafunzo kuwa mabalozi wazuri na kuwaeleza watumishi wenzao ambao hawakubahatika kupata mafunzo hayo kuyatekeleza yote waliojifunza ili kuleta ufanisi kazini.

Bi. Komba aliwataka viongozi hao kuyaishi yale yote waliofundishwa na kuyatekeleza katika maeneo yao ya kazi ili kuleta tija katika utendaji wao wa kazi za kila siku na kuongeza uwajibikaji, uwazi na uzalendo ambao utachangia katika kuboresha wao wa utendaji kazi.

Mafunzo hayo ya siku moja, yamewashirikisha Viongozi na Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze takribani 100.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >