JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

PO-ETHICS SECRETARIAT Logo
Viongozi Geita wasisitizwa matumizi ya ODS katika kujaza Tamko la Rasilimali na Madeni
20 Feb, 2026
Viongozi Geita wasisitizwa matumizi ya ODS katika kujaza Tamko la Rasilimali na Madeni

Viongozi mkoani Geita wametakiwa kutohofia matumizi ya mfumo wa ujazaji wa Tamko la Rasimali na Madeni kwa njia ya mtandao (Online Declaration System-ODS) kwani mfumo huo ni rafiki katika kutunza taarifa za mtumiaji.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela wakati akifungua mafunzo ya maadili kwa Viongozi wa Mkoa huo yaliyoandaliwa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Ziwa na kufanyika katika ukumbi wa mikuatno wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita tarehe 20 Februari, 2026.

“Utaratibu  wa kujaza fomu za  Tamko la Rasilimali na Madeni kwa Kiongozi wa Umma umewekwa kwa mujibu wa Sheria kwa Kiongozi wa Umma kujaza mali zake, na sio vinginevyo, hivyo tusiwe na hofu katika kuutumia, kwani ni mfumo mzuri hasa katika kutunza taarifa za mtumiaji,” alisema Mhe. Shigela.

Aidha Mhe. Shigela ametumia nafasi hiyo kuishukuru Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi kuendelea kuwa nao bega kwa bega kwa kuandaa semina za mara kwa mara za maadili na amewasisitiza Viongozi wa Mkoa huo kutumia semina hizo kurekebisha sehemu zenye mapungufu kwa lengo la kuimarisha ustawi wa Mkoa huo na wananchi wake.

“Tumekua tukipatiwa semina hizi kwa nyakati tofauti na mara nyingi wanakutumbusha kuwajibika kwa kufuata Sheria na kanuni zilizopo katika utumishi wa umma, hivyo ni wakati sahihi sasa kutumia semina hizi katika kuboresha sehemu zenye mapungufu kwa kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu,” aliongeza.

Awali  akiwasilisha mada kuhusu Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Ziwa Bw. Godson Kweka amewataka Viongozi wa Mkoa huo kuendelea kufanya kazi kwa pamoja, kuepuka mgongano wa maslahi na kufanya kazi bila upendeleo.

“Tusifanye kazi kwa upendeleo, ubinafsi na pia tujitaidi katika kutunza taarifa za ofisi na kuepuka vitendo vya rushwa kwa kuzingatia maslahi mapana ya wananchi,” aliongeza Bw. Kweka.

Viongozi walioshiriki mafunzo hayo ni pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Taasisi, Wakuu wa Idara na Vitengo, Wakuu wa Wilaya, Madiwani na  Kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Geita.

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >