JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Simbachawene azindua wiki ya maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu kitaifa.
05 Dec, 2024
Simbachawene azindua wiki ya maadhimisho ya siku ya  Maadili na Haki za Binadamu  kitaifa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George  Simbachewe (Mb) amezindua wiki ya maadhimisho ya siku ya Maadili na Haki za Binadamu kitaifa  kwa kufanya mkutano  na waandishi wa habari  kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini. Uzinduzi huo ulifanyika  tarehe 05 Disemba,2024 katika ukumbi wa Ofisi ya  Taifa ya Ukaguzi Jijini Dodoma.

Mhe. Simbachawene katika hotuba yake  alifafanua kuwa maadhimisho  hayo  ni  utekelezaji  wa  muunganiko  wa  siku  mbili kitaifa ambazo ni siku ya Maadili na  Haki za Biinadamu inayoadhimishwa  Disemba 10 ya kila mwaka pamoja na siku ya mapambano  dhidi ya rushwa ambayo huadhimishwa kila tarehe 9 Disemba ya kila mwaka,

Serikali ya Tanzania iliamua kuunganisha utaratibu wa Maadhimisho ya siku hizo mbili na hivyo kuifanya tarehe 10 Desemba kila mwaka kuwa siku ya Maadili na Haki za Binadamu.    

 Kauli mbiu ya maadhimisho hayo siku ha maadili na haki za binadamu kwa mwaka 2024 ni Tumia haki yako ya kidemokrasia chagua Viongozi waadilifu na wanaozingatia haki za binadamu na misingi ya utawala bora kwa maendeleo ya Taifa.

Mhe. Simbachawene alifafanua  kuwa katika kilele cha Maadhimisho ya Siku hiyo  kwa mwaka 2024 kutakuwa na  kongamano la watoa huduma ambao ni watumishi wa umma litakalofanyika katika ukumbi wa PSSF Makole tarehe 10 Disemba,2024

“Lengo la kufanya kongamano hilo kwa watumishi wa umma ni kutoa fursa kwa watumishi wa umma kujitathmini namna wanavyotoa huduma kwa kuzingatiia Maadili na Haki za Binadamu na jinsi wanavyoweza kuepuka vitendo vya rushwa katika utoaji wa huduma bora  kwa wananchi” alisema.

 

 

Katika  kongamano hilo mada mbili zitawasilishwa  na kujadiliwa ambazo ni Haki za binadamu katika mapambano dhidi ya rushwa na mada ya pili ni  Maadili haki na  wajibu wa watumishi wa Umma.

Maadhimisho  hayo yanaratibiwa na Taasisi zinazosimamia Utawala Bora nchini ambazo ni Ofisi ya Rais Ikulu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Sekretarieti ya Maadili ya  Viongozi wa Umma, Wizara ya Katiba na Sheria, Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa, Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Tume ya Utumishi wa Umma, Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali pamoja na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.

 

 

 

 

 

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >