JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

SHILINGI MILIONI 335 ZAMFIKISHA MKURUGENZI MKUU WA PSSSF MBELE YA BARAZA LA MAADILI
27 Oct, 2023
SHILINGI MILIONI 335 ZAMFIKISHA MKURUGENZI MKUU WA PSSSF MBELE YA BARAZA LA MAADILI

SHILINGI MILIONI 335 ZAMFIKISHA MKURUGENZI MKUU WA PSSSF MBELE YA BARAZA LA MAADILI

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bwana Hoseah Kashimba, amefikishwa kwenye Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma hivikaribunikwa tuhuma za ukiukwaji wa Sheria ya Maadili ikiwemo matumizi mabaya ya shilingi 335,314,803.84 fedha za mfuko.

Wakili wa Serikali Bwana Hassan Mayunga aliliambia Baraza la maadili ya Viongozi wa Ummakuwa Bwana Kashimba alitenda kosa hilo wakati akitekeleza majukumu yake ya Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF kati ya mwaka 2020 na 2021.

Alisema, “Bila kufuata taratibu mlalamikiwa alitumia fedha za Mfuko wa Hifadhi ya jamii kwa Watumishi wa Umma kiasi cha shilingi 211,671,962.00 kwa kuzikopa na kununua gari binafsi akijua kuwa fedha hizo hazikutengwa katika bajeti ya mwaka 2020/2021.”

Katika shtaka la pili, Bwana Kashimba anatuhumiwa kutumia fedha za umma katika mfuko wa PSSSF kiasi cha shilingi 123,642,841.84 kwa ajili ya kulipia kodi kama sehemu ya fedha zake za malipo ya ununuzi wa gari binafsi, kinyume na kifungu cha 6(1)(a),(b)(i) na (f) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya mwaka 1995.

Aidha Bwana Kashimba anatuhumiwa kupokea moja kwa moja fedha kutok a PSSSF kiasi cha shilingi 123,642,841.84 kwa ajili ya kulipia kodi ya ununuzi wa gari badala kodi hiyokulipwa moja kwa mojaMamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Baraza lilielezwa kuwa kitendo hicho ni kinyume na Kifungu cha 6(1)(a), (b)(i) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kikisomwa pamoja na Kanuni ya 3(2)(a)ya Kanuni za Udhibiti wa Mgongano wa Maslahi na kanuni ya 7(d) na (e) ya Kanuni za Ahadi ya Uadilifu.

“Mlalamikiwa alipokea kiasi cha shilingi 45,000,000.00 kutoka kwenye mfuko wa PSSSF ikiwa ni malipo ya samani bila kuilipia kodikinyume na kifungu cha 6(1)(a) na (c) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma,” alisema.

Mlalamikiwa alikana mashtaka yote matatu.

Katikautetezi wake Bw. Kashimba alilieleza baraza kuwafedha zote alizokopa kwa ajili ya ununuzi wa gari binafsi pamoja na kodi ni stahili yakekama Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF na hakuna taratibu au kanuni yoyote iliyokiukwa.

Vikao vya Baraza la maadili ya viongozi wa Umma ni utekelezaji wa matakwa ya Ibara ya 132 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kuhusu kusimamia tabia na mwenendo wa viongozi wa umma waliotajwa katika Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >