JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Sekretarieti ya Maadili yajipanga kutekeleza Ilani ya CCM katika eneo la Maadili.
27 Oct, 2023
Sekretarieti ya Maadili yajipanga kutekeleza Ilani ya CCM katika eneo la Maadili.

Sekretarieti ya Maadili yajipanga kutekeleza Ilani ya CCM katika eneo la Maadili.

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imejipanga kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi katika eneo la Maadili ya Viongozi wa Umma baada yakushinda uchaguzi wa 2020 nakuunda Serikali.

Hayo yalisemwa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi alipokuwa akifungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Sekretarieti ya Maadili lililofanyika 2 Machi, 2021Mjini Morogoro.

Mhe. Jaji Mwangesi alisema kuwa Katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 katika aya ya 112 ya Ilani ya Uchaguzi chama kiliahidi kuendelea kuhakikisha suala la Maadili yaViongozi wa Umma linatiliwa mkazo na kuimarishwa zaidi ili wananchi waendelee kunufaika na huduma kulingana namatarajio yao.

Kwa mujibu wa Mhe. Jaji Mwangesi ili kufikia malengo hayo Chama kiliahidi kuielekeza Serikali (Sekretarieti ya Maadili) kutekeleza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na:Kusimamia nidhamu ,uadilifu, uwazi,uzalendo wa kitaifa,moyo wa kujitolea na uwajibikaji miongoni mwa Viongozi na Watumishi wa Umma;

Mhe Jaji Mwangesi aliendelea kuyataja mambo mengine yaliyoahidiwa na Ilani nikuongeza watumishi wenye sifa stahiki kwenye utoaji huduma nakuhimiza watumishiwa umma kufanyakazi kwa juhudi, maarifa, ubunifu naweledi katika kujenga Taifa letu; Kudhibiti Migongano wa Maslahi katika shughuli za umma kwakusimamia mifumo iliyopo na Kujenga jamiii nayoheshimu na kuthamini utu, haki, maadili na nidhamu.

Kuhusu uelekeo wa taasisi katika kutekeleza majukumu yake Mhe. Jaji Mwangesi alisema kuwa Taasisi yoyote ile ni Lazima iwe na mwelekeo au malengo ya muda mrefu na mfupi katika kufikia malengo yake.

Hivyo basi Mhe. Jaji Mwangesi aliwaeleza Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekretarieti ya Maadili kuwa kwakuzingatia majukumu yake ya kikatiba na kisheria itaendelea kujikita katika Dira yake ya kuwa Taasisi yenye ufanisi na kuaminika katika kukuza na kusimamia Misingi ya Maadili ya Viongozi wa Umma nchini.

Wakati huo huo Mhe.Jaji Mwangesi alitumia fursa hiyo kuwaasa Watumishi wa Sekretarieti ya Maadili kuwa na Ushirikiano ili kuwa na Utendaji wenye tija katika Taasisi

“Kila mmoja ni lazima aione Idara/Kitengo au Ofisi ya Kanda ina umuhimu sawa na nyingine; Mguu unapochafuka mkono usisite kuusafisha sote tunajenga nyumba moja hakuna haja ya kugombea fito” alisisitiza Mhe.JajiMwangesi.

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliunda Baraza la Wafanyakazi tarehe 14 Januari, 2005 ikiwa ni utekelezaji wa Waraka wa Rais Namba moja wa mwaka 1970,Waraka ambao Baba wa Taifa Hayati Mwl.Julius Nyerere aliagiza kilaTaasisi ya Umma iwena Baraza la Wafanyakazi mahali pa kazi ili kuimarisha zaidi matumizi ya Dhana ya Utatu baina ya Serikali, Mwajiri na Wafanyakazi.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >