JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Sekretarieti ya Maadili yaanza kazi ya marekebisho ya Kanuni za Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma,1995
27 Oct, 2023
Sekretarieti ya Maadili yaanza kazi ya marekebisho ya Kanuni za Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma,1995

Sekretarieti ya Maadili yaanza kazi ya marekebisho ya Kanuni za Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma,1995

Sekretarieti ya Maadili imeanza kazi ya kufanya marekebisho ya Kanuni za sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Namba 13 ya mwaka 1995, Katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Edema mkoani Morogoro kuanzia tarehe 06 Juni 2022 hadi tarehe10 Juni 2022.

Akifungua kikao kazi hicho kwa niaba ya Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi ,Katibu Idara ya Ukuzaji Maadili Sekretarieti ya Maadili Bw. Waziri Kipacha alisema kuwa kazi hii ya urekebu wa kanuni za Maadili inafanyika kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Bw. Kipacha alieleza kuwa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma tokea kutungwa kwake mwaka 1995 imetungiwa kanuni zipatazo nne pamoja na kutolewa matangazo ya Serikali mawili kwa lengo la kuongeza ufanisi na kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya Sekretarieti ya Maadili.

Aidha Bw. Kipacha aliongeza kuwa Kanuni hizo ni Pamoja na Kanuni za Tamko la Rasilimali, Maslahi na Madeni za mwaka 1996,Kanuni za Mwenendo wa Uchunguzi katika Baraza la Maadili za mwaka 2017, Kanuni za Udhibiti wa Mgongano wa Maslahi za mwaka 2020 na Kanuni za Ahadi ya Uadilifu za mwaka 2020.

“ Kwa kuwa yemekwisha fanyika marekebisho ya Sheria mwaka 2001 na mwaka 2016 na pia kufanyika kwa marejeo hadi mwaka 2020 na kuibuka kwa mahitaji mapya ya Taasisi , Sekretarieti inalazimika kufanya marekebisho katika kanuni zate tajwa ili kuendana na mahitaji ya Taasisi kwa wakati ulipo” alisema Bw. Kipacha

Bw, Kipacha alitoa wito kwa washiriki wa kikao kazi hicho kushiriki kikamilifu na kutoa michango muhimu katika kazi hiyo kwani washiriki hao ni wazoefu na wabobevu wa fani ya sheria na ni sehemu ya watekelezaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Kanuni zake zote.

“Nawakumbusha kuwa kazi hii ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Mapambano dhidi ya Rushwa, awamu ya 111( NASCSAP-111), na hivyo ni sehemu ya kipimo kwa Taasisi yetu katikautekelezaji wa mpango huo na baadae tutatolea taarifa ya utekelezaji kwenye mamlaka husika” alifafanua Bw. Kipacha.

Kazi hii yamarekebisho ya Kanuni za Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, 1995 itakua na faida kubwa kwa Taasisi kwani kinachofanyika kinaenda kurahisisha na kuimarisha utendaji kazi wa Taasisi na utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >