JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma yahitimisha wiki ya Utumishi wa Umma.
27 Oct, 2023
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma yahitimisha wiki ya Utumishi wa Umma.

Katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili imefanya ziaraya kutembelea kituo cha kulelea watoto yatima cha Kijiji cha Matumaini pamoja na kufanya usafi katika Soko Kuu la Majengo lililopo jijini Dodoma.

Katika ziara hiyo, watumishi wa Sekretarieti ya Maadili wamekabidhi mahitaji mbalimbali katika Kituo cha watoto yatima zikiwemo sabuni na ‘pampers’ kwa watoto hao pamoja na vifaa vya kufanyia usafi kwa Soko Kuu la Majengo.

Akizungumza kwa niaba ya Kamishna wa Maadili wakati wa kukabidhi misaada hiyo, Katibu Idara ya Usimamizi wa Maadili Bw. John Kaole alisema, “Tumekuja kushirikiana na nyie kukuza Maadili ya jamii kwasababu maadili yanaanzia katika ngazi ya chini.”

Bw. Kaole aliongeza kuwa kituo hicho kinafanya kazi nzuri ya kuisaidia Sekretarieti ya Maadili kupata viongozi bora waliolelewa kwa kuzingatiamaadili.

Aidha Katibu huyo alifafanua kuwa watumishi wameguswa sana na kazi kubwa inayofanya na masista wa Shirika la ASC wanaotunza watoto hao yatima ndio maana wamekuja kuwapa faraja.

“Tunawapongeza sana Watawa mnaosimamia kituo hiki cha kijiji cha matumaini, mnalea watoto hawa kwa upendo, lakini zaidi ya yote mnawasaidia na kuwalea kwa upendo mkubwa na kuhakikisha wanapata mahitaji yote ya kijamii ikiwemo elimu,” alisema.

Kwa upande wake Makamu Mkurugenzi wa kituo hicho Sr. Suzana Maingu alitoa shukrani kwa Sekretarieti ya Maadili kwa upendo mkubwa wa kuwatembelea na kujitoa kwa ajili ya watoto hao.

“Napenda kuishukuru Sekretarieti ya Maadili na nyote mliofika hapa kutoa msaada kila mmoja kwa nafsi yake kwa majitoleo yenu nakutambua uwepo wetu Mungu awabariki sana,” alisema.

Matembezi hayo ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma ambayo ilianza kuanzia tarehe 16 june ambapo kilele chake ni tarehe 23 Juni 2021 .

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >