JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma yaanza kuitafsiri Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya 1995.
27 Oct, 2023
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma yaanza kuitafsiri Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya 1995.

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imeanza kutekeleza kwa vitendo takwa la kisheria la kuitafsiri Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma linalotokana na marekebisho kwenye kifungu cha 84(1) na (2) cha Sheria ya Tafsiri za Sheria (Interpretation of Laws Act).

Kazi hiyo inayofanywa kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali inafanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Edema, mjini Morogoro kuanzia tarehe 27 – 31 Desemba, 2021.

Akifungua kikao kazi hicho kwa niaba ya Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi, Katibu – Idara ya Ukuzaji Maadili, Sekretarieti ya Maadili Bw. Waziri Kipacha alisema kuwa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Sura ya 398 ilitungwa kwa lugha ya kingereza na hapakuwa na nakala rasmi iliyo kwenye lugha ya Kiswahili na hata iliyopo haikupitia utaratibu rasmi unaotamabulika.

Kwa mujibu wa Bw. Kipacha, mwaka huu yamefanyika marekebisho kwenye kifungu cha 84(1) na (2) cha Sheria ya Tafsiri za Sheria (Interpretation of Laws Act), Sura ya 1, kupitia kifungu cha 4 cha the Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act, Na. 1 ya 2021 na kuagiza kuwa lugha ya Sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zitakuwa ni Kiswahili pamoja na Sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambazo kwa sasa zipo kwa lugha ya Kingereza zitatafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili.

Bw. Kipacha aliendelea kubainisha kuwa kutokana na marekebisho hayo kuweka takwa la kufasiri Sheria zote kwenye lugha ya Kiswahili ikaonekana ni vema kufanya sasa kazi hii ya kutafsiri Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma sasa kwa ufadhili wa Serikali ya Uingereza kupitia Mradi wa kuzijengea uwezo Taasisi katika kupambana na rushwa nchini Tanzania.

Bw. Kipacha alitumia fursa hiyo kuwataka washiriki wa kazi hiyo ambao wengi wao niwanataaluma ya sheria kwa ngazi ya shahada na kuendelea, kutumia taaluma zao za sheria na kuwatumia vizuri Maafisa kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupitia Kurugenzi ya Uandishi wa Sheria ili waweze kupata kitu kizuri.

“Nawakumbusha kuwa kazi hii ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Mapambano dhidi ya Rushwa, awamu ya III (NACSAP-III) hivyo ni sehemu ya kipimo kwa Taasisi yetu katika utekelezaji wa mapango huo na baadae tutatolea taarifa ya utekelezaji kwenye mamlaka husika” alifafanua Bw. Kipacha.

Uwepo wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa lugha ya Kiswahili utawasaidia wadau wake hususani wananchi wa kawaida kuifahamu Sheria hii kwa lugha wanayoifahamu hivyo kuisaidia Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma katika kusimamia utekelezwaji wake.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >