JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

PO-ETHICS SECRETARIAT Logo
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kushirikiana na vyombo vya habari katika kukuza maadili
30 Mar, 2026
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kushirikiana na  vyombo vya habari katika kukuza maadili

Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imekutana na kufanya kikao kazi na wadau wa habari wakiwemo wamiliki wa vyombo vya habari, wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa lengo la kuimarisha uhusiano katika kukuza maadili nchini.

Kikao kazi hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Midland iliyopo Makambako mkoani Njombe tarehe 30 Machi, 2026.

Akifungua hicho Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Bw. Pauline Kanoni amesema lengo la kikao hicho ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari katika kuchakata na kuripoti habari zenye viashiria vya ukiukwaji  wa maadili hasa kwa Viongozi wa Umma na pia kuimarisha uhusiano kati ya ofisi hiyo na vyombo vya habari vya mikoa hiyo.

“Tumewaita hapa kwa lengo la kujadiliana namna ya kuripoti habari kuhusu Viongozi wa Umma hasa wanapokiuka maadili katika uwajibikaji wao, maana vyombo vya habari ni nyenzo muhimu katika kutoa taarifa zenye viashiria vya ukiukwaji wa maadili, na pia ni mhimili katika kukuza uhusiano kati ya Serikali na wananchi,” alisema Bw. Kanoni.

Aidha Bw. Kanoni ameongeza kuwa katika ushirikiano huo vyombo vya habari vitanufaika katika kupata elimu ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma kupitia semina mbalimbali kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wao vyombo vya habari watakua na jukumu la kuandaa na kutoa muda kwa ajili ya taarifa mbali mbali kuhusu uadilifu kwa Viongozi wa Umma na jamii kwa ujumla.

“Kama tunavyojua Serikali ina vyombo vyake vya habari, lakini tukitegemea vyombo hivyo pekee hatuwezi kufikia lengo la kuwajulisha wananchi kazi za Serikali yao kwa upana na kwa wakati ,hivyo kupitia ushirikiano huu tutawafikia wananchi wengi na wao kupata kujua yanayofanywa na Serikali yao,’’ aliongeza.

Akitoa neno la shukrani, mmiliki wa kituo cha redio ya Ice Fm iliyopo Makambako mkoani Njombe Dkt. Yono Kevela amesema kuwa wao kama wadau wa habari wamepokea vizuri ushirikiano huo na kuaidi kufanyia kazi yote waliokubaliana na kuomba vikao hivyo viwe endelevu.

“Tumefarijika kwa ujio wenu na tunashukuru kwa semina hii na tutafanya kazi kwa pamoja kwa ustawi mpana wa Taifa na sisi kama vyombo vya habari tutajaribu kufichua na kutoa habari za Viongozi wasiotenda haki kwa wananchi,” alisema Dkt. Kevela.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >