JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

PO-ETHICS SECRETARIAT Logo
Sekretarieti ya Maadili kushirikiana na Vyombo vya habari kukuza Maadili Nchini
01 Apr, 2026
Sekretarieti ya Maadili kushirikiana na Vyombo vya habari kukuza Maadili Nchini

Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kati - Dodoma imekutana na kufanya kikao kazi na wadau wa habari wakiwemo wamiliki wa vyombo vya habari,  wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Dodoma na Singida kwa lengo la kuimarisha uhusiano kati ya  Sekretarieti na vyombo vya habari  katika kukuza  na kuimarisha maadili  nchini.

Kikao kazi hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Zabibu  Hotel  iliyopo Mkoani Dodoma tarehe 01 Aprili, 2026.

Akifungua kikao kazi hicho Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kanda ya Kati Bi. Jasmin Awadh alieleza kuwa vyombo vya habari ni kiungo muhimu kati ya Serikali na wananchi na pia  vyombo vya habari vina mchango mkubwa katika kukuza na kuimarisha maadili nchini kupitia redio, luninga, magazeti pamoja mitandao ya kijamii.

Bi.Jasmin alifafanua kuwa jamii hupata taarifa, elimu na uelewa kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo uwajibikaji wa viongozi wa Umma.  “ katika muktadha huo vyombo vya habari vina nafasi kubwa na ya kipekee sana katika jamii yetu” alisema.

Katika hatua nyingine katibu huyo alifafanua kuwa ushirikiano wa Sekretarieti na vyombo vya habari nchini  ni suala lisiloepukika kwani utasaidia kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu Maadili ya Viongozi wa Umma, Utaongeza uwajibikaji na uwazi katika utendaji wa shughuli za umma pamoja na kusaidia katika kukemea na kufichua vitendo visivyo na maadili kwa viongozi wa umma.

’’Maadili ya Viongozi wa Umma ni msingi muhimu katika kuhakikisha uwajibikaji, uadilifu na utawala bora bila maadili imara jitihada zote za maendeleo ya taifa letu haziwezi kufikia malengo yaliyokusudiwa hivyo basi niwaombe tushirikine kwa pamoja  kuhahikisha kuwa suala hili  la kukuza na kuimarisha maadili linafanikiwa’’ alisema.

Akitoa neno la shukrani mmiliki wa Manyunyu media Bw. Benny Majata alisema kuwa kikao kazi hicho kimewajengea uwezo na uelewa mkubwa juu ya majukumu yanayotekelezwa na Taasisi hiyo

“Mimi kama mdau wa habari ninaahidi ushirikiano wa kina na Sekretarieti ya Maadili katika kuhakikisha kwamba malengo ya Taasisi na Serikalikwa ujumla yanatimia” alisema.

 

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >