JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Rasimu ya mkataba wa huduma kwa mteja kujadiliwa.
27 Oct, 2023
Rasimu ya mkataba wa huduma kwa mteja kujadiliwa.

Wadau mbalimbali kutoka Sekta mbalimbali nchini, wamekutana kujadili rasimu ya mkataba wa huduma kwa mteja wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma tarehe 07 Novemba, 2022.

Akifungua Mkutano huo Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Sivangilwa Mwangesi alisema kuwa Sekretarieti imeona ni vyema kuwakutanisha wadau hao muhimu kushiriki katika kutoa maoni na mapendekezo mbalimbali ya namna bora ya kuboresha utoaji huduma kwa wateja wao.

Mhe. Kamishna alifafanua kuwa mkataba wa huduma kwa mteja ni mwongozo unaoilazimisha Taasisi kutekeleza majukumu yake katika viwango vya juu vinavyokubalika. “Tumewaiteni leo ili kupata mapendekezo yenu ambayo yatakua ndio msingi wa mkataba huu” alisema.

Katika hatua nyingine Mhe. Kamishna aliwasihi washiriki wa mkutano huo kutoa michango yao ya hali na mali ili kupata mkataba wa huduma kwa mteja ulio bora.” Ni matumaini yangu kuwa wajumbe wote mtashiriki kikamilifu katika kutoa maoni yatakayowezesha kupata mkataba wa huduma kwa mteja ulio bora, unaokidhi matakwa na matarajio ya wateja ambao ndio ninyi na wengine mnaowawakilisha hapa leo” alisema.

Rasimu hiyo ya mkataba wa huduma kwa mteja imeandaliwa na timu ya watumishi wa Sekretarieti ya Maadili ya viongozi wa umma kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora.

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >