JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS – SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Rais Samia aliagiza Baraza la Maadili kuanza kazi kwa kuangalia kesi za maadili katika utumishi wa umma.
27 Oct, 2023
Rais Samia aliagiza Baraza la Maadili kuanza kazi kwa kuangalia kesi za maadili katika utumishi wa umma.

Rais Samia aliagiza Baraza la Maadili kuanza kazi kwa kuangalia kesi za maadili katika utumishi wa umma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka wajumbe wa Baraza la Maadili kuanza kazi mara moja kwa kuangalia kesi za maadili zilizoko katika utumishi wa umma zitakazo wasilishwa katika Baraza hilo.

Amesema hayo baada ya kuwaapisha wajumbe wa Baraza la Maadili Aprili2, 2022 katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

Wajumbe wa wa baraza hilo walioapishwa ni Mwenyekiti wa Baraza Jaji (Mst) Mhe. Ibrahimu Mipawa, Bw. Peter Ilomo na Bi Suzan Mlawi. Hafla hiyo iliudhuriwa pia na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson pamoja na viongozi wengine wa Serikali.

Kwamujibu wa Mhe. Rais, “mambo mengi yanatokea serikalini kwasababu hakuna Baraza la Maadili, hivyo nimeona muape na muanze kazi.”

Alieleza kuwa kesi nyingi za watumishi wa umma zinapelekwa katika taasisi nyingine za umma badala yakusikilizwa na Baraza kutokana na Baraza kutokuwepo.

“Sijawahi kupokea taarifa ya Baraza. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma inafanyaje kazi kamaBaraza lililoteuliwa mwaka 2019 halijaapa? Nimeona muape na kuanza kazi.”

Online Help
Kuanzisha Enzi Mpya katika Udhibiti wa Sekta ya Michezo ya Kubahatisha nchini Tanzania
Ofisi ya maadili inafanya kazi na imewashughulikia viongozi wengi sana kupitia Baraza la Maadili ambalo pia liliendeshwa mwaka 2013 Novemba mkoani Tabora. Viongozi mbalimbali waliokuwa na tuhuma za ukiukaji wa maadili waliitwa kwenye Baraza na kuhojiwa na Baraza linatoa mapendekezo na kuyawasilisha mapendekezo hayo kwa Rais kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu na kisheria kwa viongozi husika.

" >
Kifungu cha 11(1) cha Sheria ya Maadili kimeainisha wazi mali zinazotakiwa kutajwa kuwa ni fedha taslimu, fedha zilizopo katika taasisi za kifedha kama vile benki, hisa, nyumba, mashamba, magari, mitambo na mali nyinginezo. Kiongozi anatakiwa kutoa tamko la mali anazomiliki yeye mwenyewe, mke/mume na watoto walio chini ya umri wa miaka kumi na nane. Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni zinatakiwa kujazwa kila mwaka na kiongozi hutumiwa fomu hizo na Ofisi ya Maadili na pia zinapatikana katika mtandao wa maadili yaani www.ethicssecretariat.go.tz. Sheria inamtaka kiongozi kutolea tamko madeni yake ili kuweza kujua kuwa kiongozi anamiliki mali zipi na pia kutambua kuwa amezipata vipi mali hizo ukilinganisha na kipato cha kiongozi husika. Kiongozi kuwa na mali nyingi si dhambi kwani hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kumiliki mali ila ofisi inataka kujiridhisha uhalali wa jinsi mali ilivyopatikana. Mapendekezo katika Katiba mpya yanasisitiza maadili kwa kutenganisha uongozi na biashara.

" >
Wananchi wengi wamejijengea dhana kuwa bila pesa huwezi kupata huduma ya kiserikali kitu ambacho si kweli kwani huduma nyingi za kiserikali zinatolewa bure kabisa ila cha msingi wananchi wanatakiwa kutoa taarifa katika vyombo husika pindi wanapotakiwa kulipia huduma ambazo zinatolewa bure. Jamii inatakiwa kubadilika na kuamini kuwa si lazima kutoa rushwa ndipo upate huduma. Wapo wananchi wengi ambao walileta malalamiko kama hayo na Ofisi ya Maadili iliyashughulikia, hivyo wananchi wasisite kutembelea Ofisi zetu kwa ajili ya kutoa taarifa kama hizo.

" >
Kutoa lugha chafu ni ukiukwaji wa maadili. Ndani ya Bunge kuna Kamati ya Maadili ambayo ipo kwa ajili ya kuwawajibisha wabunge wanaotoa lugha chafu. Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa upande wake ilifanya semina kwa wabunge ili kuwakumbusha mipaka ya utendaji kazi na maadili kwa ujumla, na tangu wakati huo matumizi ya lugha chafu bungeni yamepungua kwa kiasi kikubwa.

" >